Mkurugenzi wa Mifumo ya Malipo Benki Kuu, Bw. Bernard Dadi (kushoto)
akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari mwishoni mwa wiki jijini Dar es
Salaam wakati wa kutangaza rasmi mabenki kufanya kazi kwa muda wa nyongeza
kuwawezesha wateja wa bandari na wadau wengine kufanya malipo hadi saa 2 usiku
kwa siku za kazi na saa 8 kwa siku za mwisho wa wiki na sikukuu. Wengine ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es
Salaam, Bw. Hebel Mhanga (wa pili kushoto), Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya
Uchukuzi, Bw. Gabriel Migire (wa pili kulia) na Kamishna wa Forodha wa TRA, Bw.
Tiagi Kabisi (kulia). Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza ufanisi bandari hiyo.
Kaimu
Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Hebel Mhanga (kulia) akielezea
jambo kwa kundi la waandishi wa habari waliotembelea bandari
hiyo kuona maendeleo ya utekelezwaji wa miradi inayotekelezwa chini ya
mpango
wa Matokeo Makubwa Sasa mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Inatarajiwa kuwa baada ya kukamilika, miradi
hiyo itaongeza uwezo na ufanisi wa bandari hiyo.
Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Hebel Mhanga (kulia)
akiteta jambo na Mkurugenzi wa Mifumo ya Malipo Benki Kuu, Bw. Bernard Dadi mwishoni
mwa wiki jijini Dar es Salaam wakati wa kutangaza rasmi mabenki kufanya kazi
kwa muda wa nyongeza kuwawezesha wateja wa bandari na wadau wengine kufanya
malipo hadi saa 2 usiku kwa siku za kazi na saa 8 kwa siku za mwisho wa wiki na
sikukuu. Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza
ufanisi bandari hiyo.
Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imeelezea
kuridhishwa kwake na uamuzi wa serikali kuruhusu rasmi nyongeza ya muda wa
kufanya kazi kwa benki hapa nchini na kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuongeza
ufanisi wa bandari ya Dar es Salaam.
Hatua hii inakuja baada ya serikali kupitia Benki Kuu ya
Tanzania (BoT) kuruhusu kutumika kwa mfumo wa huduma baina ya taasisi za
kibenki (TISS) hadi saa 2 usiku na hivyo kuwezesha wateja kufanya malipo na kuendelea
na taratibu nyingine katika bandari hiyo bila tatizo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...