KUSOMA  ZAIDI  links  goes  to  sheriayakub.blogspot.com
Na  Bashir  Yakub.
KISHERIA  haizuiwi  kuweka  rehani  nyumba  ya  makazi  kwa  ajili  ya  kupata  mkopo  kutoka  taasisi  yoyote  ya  fedha. Jambo la msingi  sana  ni  kuwa  watoa  mkopo   wajiridhishe   na  umiliki  wa  nyumba  hiyo  hasa  kwa  kuangalia ikiwa  ni  mali  ya  familia  au  hapana ili wachukue  hadhari  za  kisheria.

Nyumba  ya  makazi  ni  ipi.  Nyumba  ya  makazi  ni  ile  nyumba  ambayo  inatumiwa  na  binadamu  kuishi  lakini  zaidi  wanaoishi  mle  ndani  iwe  ni  familia  ya  mchukua  mkopo.  Yawezekana  nyumba  ikawa  ni  ya makazi kwa  watu  wengine  lakini  ni  ya  biashara  kwa  mchukua  mkopo. Kwa  mfano  nyumba  za  kupanga  ambapo  mwenye  nayo  anaishi  kwingine   na nyumba  iko  kwingine ikiwa  na  watu  wengine.

 Nyumba  ya  namna  hii  haitaingia  kwenye  nyumba  ya  makazi  kwa  tafsiri  hii.  Hata  hivyo  haitarajiwi  mchukua  mkopo  kuhamia  kwenye  nyumba  ambayo  sio  ya  makazi  kwa  makusudi  na kuifanya  ya  makazi  akilenga   kuhadaa  ili  kupata  upendeleo  wa  mahakama.  Akifanya  hili  atakuwa  amedanganya  na  ni  kosa  kama  tutakavyoona.

1.MAKOSA  YA  KISHERIA  KWA  MKOPAJI.
( a ) Sheria  ya  masuala  ya  rehani  ya  2008  inamtaka  mkopaji  kutofanya  udanganyifu  wa  aina  yoyote  kwa  taasisi inayotarajia  kumpa mkopo. Moja  ya  udanganyifu  ni  kama  ilivyoelezwa  hapo  juu  lakini  pia  upo  udanganyifu  mwingine  mwingi  ambao hufanywa  na  wakopaji. Kwa  mfano  kuweka  rehani  nyumba  moja  kwa  taasisi  tofauti,  kudanganya  nyumba  sio  ya  familia  wakati  ni  ya  familia  na  udanganyifu  mwingine  mwingi  ambao  hulenga  kumnufaisha  mkopaji.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...