Afisa vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw.Godfrey Massawe akizungumza na wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa kabla ya kufunga mafunzo ya wawezeshaji hao leo Jijini Mwanza.
 Mwezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha Bi. Virginia Chacha (kulia) akifanya mazoezi ya uwezeshaji kwa wawezeshaji wenzake kama njia mojawapo ya kupima uwezo wa wawezeshaji hao kabla ya kufunga Mafunzo ya Uwezeshaji leo Jijini Mwanza
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bibi. Susan Ndunguru (wapili kushoto waliokaa) katika picha ya pamoja na Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha baada ya kufunga mafunzo ya uwezeshaji leo Jijini Mwanza. Wapili kulia ni Mtaalam wa Stadi za Maisha Bw. Benny Lugoe na wakwanza kulia ni Afisa Vijana Bw. Godfrey Massawe.
Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo, Mwanza


Na: Genofeva Matemu - Maelezo, Mwanza
Vijana wametakiwa kutumia vizuri mazingira wanayowazunguka kuibua mbinu mbalimbali za ujasiriamali ili kuweza kuondoka na taifa tegemezi kwa kusubiri kuajiriwa mara baada ya  kuhitimu masomo yao.

Rai hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bibi. Susan Ndunguru alipokua akifunga mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha leo Jijini Mwanza.

Bibi. Ndunguru amesema kuwa vijana waliopata mafunzo ya uwezeshaji wa stadi za maisha ni mabalozi ambao kama watatumia vizuri uwezo walioupata katika mafunzo hayo watabadili fikra za vijana wengi nchini hivyo kuweza kujenga taifa lenye afya nzuri, weledi na pamoja na ujuzi.

KWA PICHA ZAIDI BOFY HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...