Afisa
vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw.Godfrey Massawe
akizungumza na wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha kutoka Mikoa ya Kanda
ya Ziwa kabla ya kufunga mafunzo ya wawezeshaji hao leo Jijini Mwanza.
Mwezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha Bi. Virginia Chacha (kulia) akifanya
mazoezi ya uwezeshaji kwa wawezeshaji wenzake kama njia mojawapo ya kupima
uwezo wa wawezeshaji hao kabla ya kufunga Mafunzo ya Uwezeshaji leo Jijini
Mwanza
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bibi. Susan Ndunguru (wapili kushoto waliokaa)
katika picha ya pamoja na Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha baada ya
kufunga mafunzo ya uwezeshaji leo Jijini Mwanza. Wapili kulia ni Mtaalam wa
Stadi za Maisha Bw. Benny Lugoe na wakwanza kulia ni Afisa Vijana Bw. Godfrey
Massawe.
Picha
na:
Genofeva Matemu – Maelezo, Mwanza
Na:
Genofeva Matemu - Maelezo, Mwanza
Vijana wametakiwa
kutumia vizuri mazingira wanayowazunguka kuibua mbinu mbalimbali za
ujasiriamali ili kuweza kuondoka na taifa tegemezi kwa kusubiri kuajiriwa mara
baada ya kuhitimu masomo yao.
Rai hiyo imetolewa na
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bibi. Susan Ndunguru alipokua akifunga
mafunzo ya Wawezeshaji wa Kitaifa wa Stadi za Maisha leo Jijini Mwanza.
Bibi. Ndunguru
amesema kuwa vijana waliopata mafunzo ya uwezeshaji wa stadi za maisha ni
mabalozi ambao kama watatumia vizuri uwezo walioupata katika mafunzo hayo
watabadili fikra za vijana wengi nchini hivyo kuweza kujenga taifa lenye afya
nzuri, weledi na pamoja na ujuzi.
KWA PICHA ZAIDI BOFY HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...