Waandsihi wakimsikiliza Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), Profesa Yunus Mgaya katika mkutano na waandsihi wa habari uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii/Picha na Cathbert Kajuna.
WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Tume ya Vyuo Vikuu nchini ,Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) pamoja na Kamati ya Wakuu wa vuo Vikuu nchini (CVCPT) imeandaa kongamano la saba la elimu.
Akizungumza na waandishi habari leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), Profesa Yunus Mgaya amesema wazo la kuandaa makongamano ya elimu ya juu nchini ni kubadilishana uzoefu na maarifa miongoni mwa wadau elimu katika mstakabali wa taifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...