Kamishna Msaidizi wa Madini, Kanda ya Kati – Magharibi, Humphrey Mmbando akitoa ufafanuzi wa baadhi ya masuala muhimu yaliyojitokeza wakati wa semina kwa wachimbaji wadogo wa madini kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji wa leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP). Semina hiyo imefanyika leo mjini Shinyanga na ni mwendelezo wa Mafunzo yanayotolewa nchi nzima kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchini. Wengine pichani (mstari wa mbele) ni baadhi ya Maofisa kutoka Ofisi ya Madini – Shinyanga.
 Baadhi ya akina mama ambao ni wachimbaji wadogo wa madini mkoani Shinyanga wakiwa katika semina kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP). Kutoka Kushoto ni Amina Mtoro, Hafsa Issa, Halima Mohamed, Khadija Salum na Nusura Juma. Semina hiyo imefanyika leo mjini Shinyanga na ni mwendelezo wa Mafunzo yanayotolewa na Wizara ya Nishati na Madini kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchi nzima.
 Mtaalamu kutoka Kitengo cha Leseni cha Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Nuru Shabani, akitoa ufafanuzi kuhusu utaratibu wa utoaji wa leseni kwa njia ya mtandao wakati akiwasilisha mada kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP) kwa wachimbaji madini wadogo, wakati wa Semina maalumu iliyofanyika leo Septemba 9, 2015 mjini Shinyanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...