Kamishna Msaidizi wa
Madini, Kanda ya Kati – Magharibi, Humphrey Mmbando akitoa ufafanuzi wa baadhi
ya masuala muhimu yaliyojitokeza wakati wa semina kwa wachimbaji wadogo wa
madini kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji wa leseni za madini kwa njia ya
mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP). Semina hiyo
imefanyika leo mjini Shinyanga na ni mwendelezo wa Mafunzo yanayotolewa nchi
nzima kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za madini nchini. Wengine
pichani (mstari wa mbele) ni baadhi ya Maofisa kutoka Ofisi ya Madini –
Shinyanga.
Baadhi ya akina mama
ambao ni wachimbaji wadogo wa madini mkoani Shinyanga wakiwa katika semina
kuhusu mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa njia ya mtandao
(Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP). Kutoka Kushoto ni Amina
Mtoro, Hafsa Issa, Halima Mohamed, Khadija Salum na Nusura Juma. Semina hiyo
imefanyika leo mjini Shinyanga na ni mwendelezo wa Mafunzo yanayotolewa na
Wizara ya Nishati na Madini kwa wachimbaji wadogo na wamiliki wa leseni za
madini nchi nzima.
Mtaalamu kutoka Kitengo
cha Leseni cha Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Nuru Shabani, akitoa
ufafanuzi kuhusu utaratibu wa utoaji wa leseni kwa njia ya mtandao wakati akiwasilisha
mada kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa huduma za utoaji leseni za madini kwa
njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal – OMCTP) kwa wachimbaji
madini wadogo, wakati wa Semina maalumu iliyofanyika leo Septemba 9, 2015 mjini
Shinyanga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...