Dar
es Salaam, TANZANIA. Leo asubuhi, Balozi
wa Tanzania nchini Tanzania Mark Childress amewaapisha wafanyakazi wa
kujitolewa wa Kimarekani (Peace Corps Volunteers) wapatao 59 ili kuanza huduma
yao ya miaka miwili nchini Tanzania. Hafla ya kuwaapisha wafanyakazi hao
ilifanyika katika viwanja vya Ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam na
kuhudhuriwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ukaguzi wa Shule ya Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Edicome Cornel Shirima, Mkurugenzi Mkazi wa
Peace Corps nchini Tanzania Dk. Elizabeth O’Malley, watu waliowahi kuwa
wafanyakazi wa kujitolea wa Peace Corps katika sehemu mbalimbali duniani na
maafisa wa taasisi wabia wa kiserikali na taasisi nyingine za kujitolea.
Katika
hotuba yake, Balozi Childress aliwaambia wafanyakazi hawa wapya wa kujitolea wa
Peace Corps kuwa “Mojawapo ya maneno yanayonivutia sana ninayoyasikia mara kwa
mara nchini Tanzania ni neno pamoja.
Neno hili linawasilisha moyo wa ushirikiano baina ya nchi zetu mbili na
miongoni mwa Watanzania. Na hivi sasa mnapoanza safari na rafiki na wabia wenu
wa Kitanzania, ninachoweza kuwaambia kuwa kwa pamoja mtakuwa na safari yenye kusisimua sana.”
Katika
hotuba yake kwa wafanyakazi wapya wa kujitolea Dk. Shirima alirejelea maoni ya
Balozi, akiwaasa kuwa “fanyeni kazi kwa bidii, fanyeni yaliyo mema, yafanyeni
hayo kwa moyo wote, enzini uzoefu mtakaoupata na kuhusiana vyema na watu wa
Tanzania. Kwani mtakuwa mkiishi na kufanya nao kazi bega kwa bega katika shida na raha. Furahieni
muda wenu mtakaokuwa hapa Tanzania.”
Naye
Mkurugenzi Mkazi wa Peace Corps Dk. Elizabeth O’Malley alisema “Kwa niaba ya Peace
Corps Tanzania, ninapenda kutambua na kushukuru kwa ushirikiano mkubwa
tunaoendelea kuupata kutoka kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
kwa upande wa Zanzibar na Bara, hususan kutoka kwa Wizara za Elimu na Mafunzo
ya Ufundi, Menejimenti ya Utumishi wa Umma katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI na
Wizara ya Afya. Aidha, napenda
kuwashukuru Maafisa Elimu wa Wilaya na Wakuu wa Shule wanaotoa msaada mkubwa
kwa watendaji wetu na wafanyakazi wetu wa kujitolea.”
Wafanyakazi
wa hawa 59 wa kujitolewa walioapishwa leo watapangiwa kufanyakazi katika wilaya
za Karatu, Kongwa, Chamwino, Mufindi, Iringa Vijijini, Hai, Rombo, Lushoto,
Wete na Nzega. Wengina watapangiwa
katika wilaya za Moshi Vijijini, Same,
Ruangwa, Nachingwea, Hanang, Babati, Kiteto, Tukuyu, Kyela, Chunya, Mbarali,
Masasi, Newala na Mtwara Vijijini. Wengine watakwenda katika wilaya za Mbinga,
Shinyanga, Kishapu, Maswa, Singida vijijini, Iramba, Nzega na Lushoto.
Wafanyakazi
hawa wa kujitolea wa kimarekani watatoa huduma kwa wanafunzi wao, shule na
jamii watakazokuwa wakiishi kwa kufundisha masomo darasani pamoja na kuendesha
miradi mbalimbali ya kijamii mathalan ile inayohusu lishe bora, stadi za
maisha, afya bora, mazingira na mafunzo ya kusoma na kuandika. Aidha, kwa miaka miwili ya kuwepo kwao hapa
nchini, wafanyakazi hawa watachangia katika jitihada za Tanzania za kuongeza
idadi ya walimu wa hisabati, Sayansi na Kiingereza hususan katika maeneo ya
vijijini.
Peace Corps ni taasisi ya
Serikali ya Marekani iliyoanzishwa na Rais John F. Kennedy mwaka 1961 ambayo
hivi sasa inahudumia zaidi ya wafanyakazi wa kujitolea zaidi ya 8,000 katika
zaidi ya nchi 75 duniani. Kwa miaka 48, Peace Corps imekuwa taasisi
inayoendesha shughuli za mabadilishano ya kiufundi na kitamaduni zisizoegemea
mrengo wowote wa kisiasa na kidini. Jumla ya wafanyakazi wa kujitolewa wapatao
189,000 wamehudumu katika nchi zipatazo 138. Peace Corps ina dhamira ya kukuza
amani na urafiki duniani kwa kutekeleza malengo matatu yafuatayo:
·
Kutoa
wafanyakazi wa kujitolea wa Kimarekani watakaochangia kuleta maendeleo ya
kijamii na kiuchumi katika nchi itakayohitaji wafanyakazi hao;
·
Kukuza
uelewa kuhusu Wamarekani miongoni mwa watu katika jamii zinazohudumiwa na
Wafanyakazi wa kujitolea;
·
Kuimarisha
uelewa wa Wamarekani kuhusu dunia na watu wake.
Zaidi ya Wafanyakazi wa
Kujitolea wa Peace Corps wapatao 2,000 wamehudumu nchini Tanzania toka mwaka
1962. Peace Corps hutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa kujitolea wa Marekani wanao
fanyakazi katika jamii katika Nyanja za elimu ya sekondari (wakifundisha
hisabati, sayansi na teknolojia ya mawasilianoa), afya na elimu ya mazingira.
Kwa taarifa Zaidi, tafadhali
wasiliana na Japhet Sanga (SangaJJ@state.gov), Afisa Habari Mwandamizi wa
Ubalozi wa Marekani
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...