Mkimbizi
kutoka Burundi, Philipo Nyandungulu, akishuka kutoka kwenye basi baada
ya kuwasili katika kambi ya
wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko Kasulu mkoani Kigoma. Idadi ya wakimbizi kutoka Burundi imekuwa ikiongezeka siku hadi siku
na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa kushirikiana na Shirika
la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wakimbizi (UNHRC) imekuwa ikiwahifadhi kwa
muda katika kambi hiyo.
Wakimbizi kutoka Burundi wakipata maelezo ya jinsi ya kuishi
katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu mkoani Kigoma
mara baada ya kuwasili kambini hapo.
Anayetoa maelekezo hayo ni Nayiga Mireye wa Shirika la Maji na Usafi wa Mazingira
(TWESA) linalofanya shughuli zake kambini hapo.
(PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI, WIZARA YA MAMBO YA
NDANI YA NCHI)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...