Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Wananchi wa Kijiji cha Kwale Wilaya ya Micheweni wakati alipowasili kuzungumza nao.
 Balozi Seif akizungumza na Wananchi na Wana
CCM wa Kijiji cha Kwale Wilaya ya Micheweni akitekeleza ahadi aliyotoa
kwa Wazee Waasisi wa Kijiji hicho ya kufika kusalimiana nao.
 Baadhi ya Wananchi na wanaCCM wa Kijiji cha Kwale
wakifuatilia Hotuba ya Balozi Seif hayupo pichani alipofika Kjijini
hapo kusalimiana nao.

MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi
amewatahadharisha Wananchi kuwa makini na Watu wanaochochea chuki
miongoni mwa Jamii jambo ambalo  Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
kamwe haitakubali kuona amani ya Nchi inachezewa kizembe.

Alisema wapo watu waliochoka na amani iliyopo nchini kwa kuanza
kushabikia cheche za kujiandaa kuwashawishi Vijana wawe tayari kufanya
fujo mara tuu baada  ya zoezi la kupiga kura kwenya uchaguzi Mkuu wa
Mwezi Oktoba mwaka huu.

Balozi Seif Ali Iddi ametoa tahadhari hiyo wakati akizungumza na
Wananchi amoja na Wana  CCM wa Kijiji cha Kwale Wilaya ya Micheweni
Mkoa wa Kaskazini Pemba akitekeleza ahadi aliyowapa wazee wa Kijiji
hicho hivi karibuni ya kuwatembelea na kusalimiana nao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...