Kulia ni Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya tamasha la Amani, Alex Msama.

Na Mwandishi Wetu
KAMATI ya Maandalizi ya Tamasha la Amani, imesema inapata wakati mgumu kuhusiana na idadi ya waimbaji ambao wanaomba kushiriki tamasha hilo litakalofanyika Oktoba 4, mwaka huu.
 
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Alex Msama amesema wiki hii kuwa idadi ya wanaoomba washiriki tamasha hilo imekuwa kubwa kuliko kawaida, ambapo hadi juzi walikuwa waombaji wamefikia 74.
 
“Tunapata maombi mengi, tunajitahidi kadri ya uwezo wetu kujipanga ili kuweza kila mmoja ashiriki, lakini tuna vigezo ambavyo tunaviangalia kwanza,” alisema.
 
Msama amesema tamasha hilo pia litashirikisha waimbaji wa nyimbo za Injili kutoka nchi kadhaa za Afrika ikiwa ni pamoja na Kenya, Uganda, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika Kusini na Zambia.


"Waimbaji wengi maarufu wa muziki wa injili watakuwepo, tumejipanga vizuri kuhakiksha tamasha hili linakuwa gumzo kila mahali.

"Wapendwa wajiandae kushiriki kwa wingi kwani watashiba kiroho kwa vile kutakuwa na waimbaji wengi wenye hamasa ya kiroho," alisema Msama.

Msama amesema lengo la kuwajumuisha wasanii hao ni kutaka kulifanya tamasha hilo lenye lengo la kuombea amani liwe bora na lenye tija kwa Taifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...