Na
Mwandishi Wetu
TAMASHA
la Amani linatarajiwa kufanyika Oktoba 4, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam na tayari wasanii mbalimbali wamepania kutoa burudani ya nguvu kwa
mashabiki watakaojitokeza.
Taarifa
kwa vyombo vya habari iliyotolewa wiki hii na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi
ya tamasha hilo,Alex Msama ilieleza kuwa wasanii hao
wamesema kuna mambo mazuri watayafanya siku hiyo.
Baadhi ya wasanii
waliotajwa kwamba watatumbuiza siku hiyo ni Sarah K, John Lissu, Rose Muhando,
Upendo Nkone, Upendo Kilahiro na Boniface Mwaitege.
Taarifa
hiyo inawakariri wasanii mbalimbali wakizungumzia tamasha hilo, huku wakitamba
kwamba mambo yatakuwa mazuri.
“Nimedhamiria
kuwapa mambo mazuri mashabiki wangu, najua watafurahi sana, watakaokuja
hawatajuta,” ni kauli ya Rose Muhando.
Naye
msanii Upendo Nkone, amewaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi na kuwa wana
imani kubwa litakuwa tamasha zuri.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...