Mkurugenzi wa Mifumo Juhn Mlingi kutoka Taasisi ya Mabasi yaendayo Haraka (Dar es Salaam Rapid Transport) akitoa ufafanuzi wa maendeleo ya ujenzi wa mradi huo kwa wafanyakazi wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) na waandishi wa habari walipokuwa katika ziara ya kukagua miundo mbinu ya mradi huo katika kituo cha Kivukoni jana jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Tanroads wakipanda  gari la Mradi  wa Mabasi yaendayo Haraka jana  jijini Dar es Salaam katika  ziara ya kukagua Miundo Mbinu ya Mradi  wa DART kabla  ya kuanza kutumika .
 Baadhi ya wafanyakazi wa Tanroads wakikagua  kituo cha mabasi yaendayo haraka kilichopo Kimara  ambacho ujenzi wake  umekamilika  kwa asilimia mia moja jana jijini Dar es Salaam.
 KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Wanaohujumu miundo mbinu walipe, na hizo pesa ziwekwe kwenye mfuko wa matengenezo ya mara kwa mara, ili hali ya vituo iendelee kuwa nzuri wakati wote.

    ReplyDelete
  2. Si haba Masha Allah! Madhali imeshaanza kiulaya ulaya, basi naamini taratibu taratibu hatimae tutafika. Hata Roma haikujengwa siku moja. Ispokuwa tuache tu ile tabia ya uharibifu usiokuwa na maana nadhani na hiyo faini ya laki tatu inaweza kusaidia kuwatia woga wale wenye tabia ya kuhujumu miundombinu mbali mbali iliyopo nchini.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...