Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa(Tanapa)Allan Kijazi  akiwa kwenye mazungumzo na Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp(katikati)aliyefika makao makuu ya Shirika hilo leo,kulia ni Katibu Msaidizi wa Ubalozi wa Uturuki,Berat Colak.
Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp(kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Tanapa,Allan Kijazi alipotembelea Makao Makuu ya shirika hilo  jijini Arusha.   
Katibu Msaidizi wa Ubalozi wa Uturuki,Berat Colak(kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa(Tanapa),Allan Kijazi alipotembelea Makao Makuu ya shirika hilo  jijini Arusha.   

Balozi wa Uturuki nchini Mhe. Yasemine Eralp amesema atawaalika wawekezaji kutoka Uturuki ili waweze kutumia fursa za uwekezaji zilizopo katika Hifadhi za Taifa nchini. Balozi Eralp alitoa ahadi hiyo alipotembelea Makao Makuu ya TANAPA jijini Arusha na kukutana na viongozi wa shirika.

Balozi Eralp amesema kuwa sekta ya utalii ni miongoni mwa vipaumbele vyake na kwamba atatumia muda wake mwingi kuhakikisha kuwa sekta hiyo inastawi na kuvutia watalii wengi nchini kutoka Uturuki.
Kusoma zaidi bofya HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...