Gazeti
la Mwananchi la Tarehe 14/9/2015 toleo namba 5529 ukurasa wa 25 liliandika
habari kuhusu Mwenge wa Uhuru chini ya kichwa cha Habari “Anayeumba Mwenge wa
Uhuru” huyu hapa
Wizara
ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo (WHVUM) ambayo ndiyo yenye dhamana ya
Mwenge wa Uhuru inapenda kuufahamisha umma kwamba habari hiyo sio ya kweli na
ni ya upotoshaji.

Wizara
ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ingependa kuufahamisha umma kuwa Mbio
za Mwenge wa Uhuru zilianzishwa rasmi mwaka 1964 na sio mwaka 1961 kama ilivyoandikwa katika
toleo lililotajwa. Ieleweke kwamba, Mbio za Mwenge wa Uhuru tangu kuanzishwa
kwake zimekuwa zikitumika katika kuwahamasisha wananchi wa Tanzania kuendelea
kujenga upendo, umoja na mshikamano wa Kitaifa bila ya kubaguana kwa misingi ya
kidini,rangi, jinsia, ukabila na itikadi za kisiasa.
Vilevile,
Mbio za Mwenge wa Uhuru zimekuwa zikitumika kuhamasisha na kuchochea shughuli mbalimbali za maendeleo ya wananchi kiuchumi
na kijamii kupitia kwenye ujumbe maalum unaotolewa kila mwaka na miradi ya
maendeleo inayobuniwa .
Wizara
pia, inapenda kuufahamisha umma wa
Watanzania kuwa michango ya fedha inayotolewa na wananchi kwa ajili ya Mbio za
Mwenge wa Uhuru si kwa ajili ya kugharamia mafuta ya Mwenge wa Uhuru
unaokimbizwa kama ilivyodaiwa na gazeti la Mwananchi. Fedha zinazochangwa ni
kwa ajili ya kugharamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambayo hubuniwa na
wananchi wenyewe. Aidha, michango hiyo
hutolewa kwa hiari kutoka kwa mwananchi
mmojammoja, Vikundi, Taasisi za Umma na Binafsi, Wadau wa Maendeleo, Serikali
Kuu na Halmashauri za Wilaya.
Kwa
Taarifa hii Wizara inasisitiza kuwa madai ya Ndugu Shaban Mwinchumu ni ya
upotoshaji na hayana uhusiano wowote na masuala ya Mwenge wa Uhuru. Pia, Ndugu
Shaban Mwinchumu hajawahi kupewa kazi ya kutengeneza Mwenge wa Uhuru anayodai
kuifanya kwa muda mrefu kupitia Wizara ya Kazi, Ajira na Manendeleo ya Vijana
kwani hakuna Wizara hiyo kwenye orodha ya Wizara za Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
Mwisho
kabisa Wizara inawataka waandishi wa habari na wahariri wa vyombo vya
habari kuandika habari kwa usahihi zenye kujenga Umoja wa Kitaifa kwa kupata
ufafanuzi wa kila upande ili habari itoe picha halisi badala ya kuegemea upande
mmoja kwani kwa kuegemea upande mmoja hupotosha jamii na si maadili ya taaluma
ya habari.
Imetolewa
na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Mimi sina chama (party) kikundi (group) au kijiwe (faction) cha siasa. Ni mpenda Tanzani yetu moja.
ReplyDeleteLakini naomba ufafanuzi (pengine, kutoka serikali au tume ya uchaguzi) kukataa habari za uwongo zinazotolewa na baadhi ya wapinzani kuwa kuwa CCM haijafanya lolote la maendeleo tangu uhuru. Huu ni uchochezi wa juu hasa unaolenga vijana wetu walozaliwa hivi majuzi ili kuikataa CCM na kuona Tanzania yetu kwa macho au darubini finyu ya wapinzani.
Kama sio maendeleo, hao wapinzani wasingejulikana. Ajabu ni kusikia akina Mbowe, Lissu, na hata Esther Bulaya, Lowassa na huyo Sumaye naye anaiga wimbo wa mdundiko wa kuidhalilisha CCM. hawa wasingejulikana leo hii kama si kwa ajili ya bidii za CCM za kuleta wote pamoja nchini. Ni mawazo ya mende kufikiria kuwa maendeleo ya nchi yanapimika kwa darubini ya uchumi wa ki-quantity; na sio vingine. Maendeleo mengine sio lazima yawe ya kiuchumi; yanaweza kuwa ya kisiasa, kijamii, kisaikolojia, na kadhalika.