Mkuu wa kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu B iliyopo wilayani
Kasulu Mkoani Kigoma, Fredrick Nisajile akiongea na wakimbizi walio katika
mpango wa kuhamishiwa kwenye kambi za Nduta, Mtendeli na Karago.Wakimbizi hao
waliopokelewa kutoka nchini Burundi hivi karibuni kwa sasa wanahifadhiwa kwa
muda katika kambi ya Nyarugusu.
Wakimbizi kutoka Burundi walioko katika Kambi ya Nyarugusu
wakiandaa mboga ya kisamvu kama walivyokutwa na mpiga picha wa Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi aliyeko katika ziara
katika kambi hiyo.
Mkimbizi Haverimana Ejide (kushoto) na mkewe Kugimana Evona
pamoja na watoto wao wakipata chakula cha mchana katika kambi ya wakimbizi ya
Nyarugusu B iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma ambapo wanahifadhiwa kwa muda
kabla ya kuhamishiwa maeneo mengine ili kupunguza msongamano uliopo katika
kambi ya Nyarugusu.
(PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI – WIZARA YA MAMBO YA
NDANI YA NCHI)
Amani itengamae kwao ili warudi nyumbani.
ReplyDelete