NA BASHIR YAKUB
Ni kawaida watu kukopeshana fedha katika shughuli za kibinadamu za kila siku hasa zile za uzalishaji. Ni kutokana na hili baadhi ya watu hujikuta wameingia katika faraka ambazo hata hivyo zinatatulika kisheria. Kwa wale ambao madeni yao hutokana na taasisi za fedha kama benki hawa huwa sio rahisi kwao kukwepa kutokana na utaratibu makini wa utoaji wa fedha wa taasisi hizo. Tatizo kubwa la kutolipana na kuleteana dharau huhusisha wadeni binafsi yaani mtu na mtu. Ni katika madeni haya ya watu binafsi ambamo msemo maarufu wa deni halifungi husikika. Ni kawaida kukuta mtu amekopeshwa na hataki kurejesha akijiamini kuwa deni halifungi. Yumkini wapambe nao husikika wakisema, asikutishe huyo deni halifungi. Kwa makala haya tutapata kujua ikiwa ni kweli deni linafunga au halifungi.
1.KESI YA MADAI.
Kesi za madai ni zile kesi zote ambazo si za jinai. Kesi za madai hazihusishi kudaiana pesa tu kama wengi wanavyojua. Hata masuala ya talaka, kudai fidia, mikataba, madai ya vitu kama nyumba, magari n.k navyo huingia katika kesi za madai. Kwa hiyo tunapojiuliza swali la ikiwa deni linafunga au halifungi tunaongelea hivi vyote. Hata hivyo tutajielekeza zaidi katika kudaiana fedha.
2. JE INARUHUSIWA KUPELEKA KESI YA MADAI POLISI ?.
Unayo haki ya kufungua shauri ikiwa kuna mtu unamdai lakini kwa sharti kuwa shauri lifunguliwe pahala stahiki. Wapo ambao hupeleka kesi za namna hii polisi japo huko si mahali pa kesi za namna hii. Polisi hujitahidi kuzitafutia ufumbuzi ambapo wakati mwingine hufanikiwa na wakati mwingine hushindwa. Ukweli ni kuwa kisheria polisi hawana ruhusa ya kushughulikia kesi za madai hasa hizi za kudaiana hela na hata mali. Ni basi tu wanaamua kuzishugulikia lakini si kazi yao kisheria. Madhara utakayoyapata utakapomfungulia kesi mdai wako polisi ni pamoja na kupoteza mda bila kupata ulichokitaka. Hii ni kwasababu mdaiwa atakapokataa kutoa ushirikiano wowote, polisi hawana la kumfanya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...