NA  BASHIR  YAKUB 
Ni  kawaida  watu  kukopeshana  fedha  katika  shughuli  za  kibinadamu za kila  siku hasa  zile  za  uzalishaji. Ni  kutokana  na  hili  baadhi  ya  watu  hujikuta  wameingia  katika  faraka ambazo  hata  hivyo  zinatatulika  kisheria. Kwa  wale  ambao  madeni  yao  hutokana  na  taasisi  za  fedha  kama  benki  hawa  huwa  sio  rahisi  kwao  kukwepa kutokana  na  utaratibu  makini  wa  utoaji  wa fedha wa taasisi  hizo. Tatizo  kubwa  la  kutolipana na  kuleteana  dharau huhusisha wadeni  binafsi yaani  mtu  na  mtu. Ni  katika  madeni  haya  ya  watu binafsi  ambamo  msemo  maarufu  wa  deni  halifungi husikika. Ni  kawaida   kukuta  mtu   amekopeshwa  na  hataki  kurejesha  akijiamini  kuwa  deni  halifungi.  Yumkini wapambe  nao  husikika  wakisema,  asikutishe  huyo  deni  halifungi. Kwa  makala  haya  tutapata  kujua  ikiwa  ni  kweli  deni  linafunga  au  halifungi.  

1.KESI  YA  MADAI.
Kesi  za madai  ni  zile kesi   zote  ambazo   si  za  jinai. Kesi  za  madai  hazihusishi  kudaiana  pesa  tu  kama  wengi wanavyojua. Hata  masuala ya  talaka, kudai  fidia, mikataba, madai  ya  vitu  kama  nyumba, magari n.k navyo  huingia  katika  kesi  za  madai. Kwa  hiyo  tunapojiuliza  swali  la  ikiwa  deni  linafunga  au  halifungi  tunaongelea  hivi  vyote. Hata  hivyo  tutajielekeza  zaidi  katika  kudaiana  fedha.

2.     JE  INARUHUSIWA  KUPELEKA  KESI  YA MADAI  POLISI ?.
Unayo  haki  ya  kufungua  shauri ikiwa   kuna mtu unamdai lakini kwa sharti kuwa   shauri  lifunguliwe  pahala stahiki. Wapo  ambao  hupeleka  kesi  za  namna  hii  polisi  japo  huko  si  mahali  pa  kesi  za  namna  hii. Polisi  hujitahidi  kuzitafutia  ufumbuzi   ambapo  wakati  mwingine  hufanikiwa  na  wakati  mwingine  hushindwa. Ukweli  ni  kuwa  kisheria  polisi  hawana  ruhusa  ya  kushughulikia  kesi   za  madai  hasa  hizi  za  kudaiana  hela  na  hata  mali. Ni  basi  tu  wanaamua  kuzishugulikia  lakini  si  kazi  yao kisheria. Madhara  utakayoyapata  utakapomfungulia  kesi  mdai  wako  polisi  ni  pamoja  na  kupoteza  mda  bila  kupata  ulichokitaka.  Hii  ni  kwasababu  mdaiwa  atakapokataa  kutoa  ushirikiano wowote,  polisi  hawana  la  kumfanya. 
Kusoma zaidi bofya HAPA                  au                  HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...