Naibu mkurugenzi mkuu wa Benki M Bi. Jacqueline Woiso akiongea na waandishi wa habari leo hii katika
ukumbi wa Hyatt Regency juu ya maandalizi ya Rotary Dar Marathon 2015 ambayo huandaliwa na
Rotary klabu za Dar es salaam kwa kushirikiana na Benki M. Mbio na matembezi ya Dar Rotary
Marathon kwa mwaka huu zitafanyika katika viwanja vya Green, Oysterbay tarehe 14 October 2015.
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa bodi ya Rotary Bi. Sharmila Bhatt, Mwenyekiti wa kamati ya
maandalizi Bi. Agnes Batengas, Makamu wa Raisi wa Rotary klabu Oysterbay Bi. Anne Saels na Rais wa
Rotary Klabu Dar North Bw. Masato Wassira.
baadhi ya washiriki wa Rotary Dar Marathon kutoka Malawi na Kenya wakifuatilia mkutano huo,
Marathon ya mwaka huu itajumuisha wakimbiaji kutoka nchi za Kenya, Rwanda, Malawi, South Africa na
Ethiopia.
Mbio na matembezi ya hisani za Dar rotary marathon yanatarajiwa kufanyika siku ya jumatano tarehe
14.10.2015 hapa jijini Dar es salaam ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa rais mstaafu mheshimiwa
Ally Hassan Mwinyi.
Mbio na matembezi hayo yameandaliwa na klabu sita za Rotary za hapa Dar es
salaam kwa kushirikiana na Benki M na kauli mbiu ya mwaka huu ni “kuponya maisha, badilisha jamii”
ambapo fedha zitakazochangishwa ziltaelekezwa katika ujenzi wa kituo cha afya hapa Dar es salaam.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...