KAMPUNI YA RELI TANZANIA(TRL)


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI (PRESS RELEASE)
 Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania TRL unachukua fursa  hii kuwaarifu abiria wa treni ya deluxe ya Jumapili Oktoba 25, 2015 kutoka Dar es Salaam kwenda  Mwanza kuwa muda wa kuondoka umesogezwa mbele kutoka saa 2 asubuhi hadi saa 2 usiku wa  siku hiyohiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo uamuzi huo umechukuliwa maalum ili kuwapa fursa Abiria waliojiandikisha kupiga kura kutumia haki yao ya kikatiba kikamilifu.

Utaratibu huu utatumika pia kwa treni kwa siku hiyo zitakazokuwa zinaanza safari zake kutoka Kigoma na Mwanza kuja Dar es Salaam nazo zitaanza safari hizo saa 2 usiku.

Wito unatolewa kwa kila mwananchi atakayepata taarifa hii muhimu amwaarifu mwenzake.

Shime kila Mtanzania ajitokeze kwenda  kutumia haki yake ya kikatiba kwa kumchagua Kiongozi mwenye sera anayoiafiki.

Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa niaba ya

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL Mhandisi Elias Mshana.

Dar es Salaam,
Oktoba 21, 2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...