Mhe.  Mahadhi J. Maalim  Naibu Waziri, Wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, akizungumza wakati wa Mkutano wa Nchi zilizonyuma kimaendeleo ( LDCs) wakati wa mkutano wa Mawaziri wa Kundi hilo uliofanyia siku ya Alhamis hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. Nyuma ya  Naibu Waziri, ni  Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa  Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania  katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan  M. Mwinyu 

Na Mwandishi Maalum, New York
 WAKATI  kila  Nchi mwanachama wa Umoja wa Mataifa,  ikijianda kwa utekelezaji wa Ajenda 2030 ambayo  inajikita zaidi katika kuondoa umaskini pasipo kumwacha yeyote nyuma, sanjari na kuilinda Sayari Dunia. Tanzania imehimiza  haja na umuhimu  wa nchi ambazo  ziko  nyuma kimaendeleo ( LDCs) kuzungumza kwa kauli moja.

Ushauri huo umetolewa  jana Alhamis na   Mhe. Mahadhi Juma Maalim ( Mb),  Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wakati akizungumza katika mkutano wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa LDCs uliofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, sambamba na majadiliano ya  jumla ya  Mkutano wa 70 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Katika mkutano huu wa  Mawaziri wa LDCs, Bangladesh  ilikabidhiwa uenyekiti wa  Kundi hilo kutoka kwa Benin inayomaliza muda wake. Pamoja  na Kuishukuru Benin kwa kuliongoza kundi hilo vema wakati wa  uenyekiti wake Mhe. Naibu Waziri ameiahidi Bangladesh ushirikiano  kutoka Tanzania.
“ Kundi letu linawachama wengi, tutumie basi wingi wetu  kuhakikisha  kwamba tunasukuma mbele na kuteteta masuala  yanayotuhusu kwa  kuzungumza kwa sauti  moja wakati wa majadiliano na kuhakikisha kuwa ajenda tunazosimamia  kwa maslahi yetu  hazikwami.” Amesema Naibu Waziri
Aidha Naibu Waziri Mahadhi, amelikumbusha kundi hilo kuwa moja  ya lengo kuu la kundi ni kuondoka katika kundi la nchi maskini na kuwa nchi zenye uchumi  wa kati.

“ Kwa bahati nzuri  suala la kuondoa umaskini ni moja ya eneo ambalo limepewa umuhimu wa kipekee katika Ajenda 2030, hivyo ni wajibu wetu  kama LDCs, kutumia fursa hii kwa kuhakikisha kwamba, katika kipindi cha miaka 15 ijayo nchi nyingi katika kundi letu  zina-graduate na  kuwa nchi zenye uchumi wa kati”. Amesisitiza.

Mhe. Naibu Waziri amerejea  kwa kusisitiza kauli  iliyotolewa na  Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipolihutubia Baraza Kuu la 70 la Umoja wa Mataifa, siku ya  Jumanne, Kwamba utekelezaji wa Ajenda 2030 ndiyo changamoto iliyombele yetu kwa sasa na kwamba utekelezaji wake ukikwama, LDCs ndizo zitakazo athirika zaidi.

Ni kwa sababu hiyo juhudi za pamoja katika kuhakikisha utekelezaji wa  Ajenda  2030 ni mihimu na  za lazima.

Kundi la   Nchi ambazo zipo nyuma kimaendeleo na kama zinavyotambuliwa na Umoja wa Mataifa zipo 48
Ajenda 2030 ambayo ilipitishwa wakati wa mkutano wa kilele wa kisiasa uliofanyia kwa siku tatu hapa  Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa,  ni   Ajenda yenye malengo 17 ya maendeleo endelevu  yakichukua na nafasi ya Malengo ya Maendeleo ya Milenia ambayo yanafikia  ukingoni  mwaka huu wa 2015

Ajenda 2030 itaanza kutekelezwa mwakani ( 2016 )na utekelezaji wake ni wa miaka 15

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...