Na Lorietha Laurence - Maelezo.
JESHI la Polisi nchini kwa kushirikiana na Ofisi za Shirikisho la Polisi Duniani (Interpol)  kanda ya Kusini mwa Afrika,  imefanikiwa kukamata  nyara za serikali zenye thamani ya Tsh. Milioni 81 na watuhumiwa 121 wa makosa mbalimbali.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam leo Alhamisi (Oktoba 1, 2015),  Mkurugenzi wa  Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi,  Kamishna Diwani Athuman (pichani), alisema kuwa lengo la  operesheni hiyo ni  kuongeza tija katika swala  zima la kupambana na uhalifu.
“Lengo la operesheni hii ni kuongeza tija katika kupambana na hali ya uhalifu na kuweka mazingira salama kwa wananchi na nchi jirani” alisema Kamishina Athuman.
Aidha aliongeza  kuwa operesheni hiyo  ilifanyika nchi nzima  katika kanda nane  ikiwemo kanda ya Kaskazini, kanda ya juu Kusini, kanda ya ziwa, kanda ya magharibi, kanda ya Zanzibar, kanda ya kati na kanda ya kusini na kufanikiwa kukamata  vielelezo na watuhumiwa wa makosa mbalimbali.
Kamishani Athumani alisema kuwa vielelezo vilivyokamatwa  katika operesheni hiyo ni pamoja na magari mawili yaliyoripotiwa kuibiwa nchini Japan na Afrika ya kusini ,dawa za kulevya, wahamihaji haramu 7, kutoka Kenya, Burundi na Msumbiji, bidhaa zilizopigwa marufuku zenye thamani ya Tsh. Milioni 3.5  na madini yenye thamani ya Tsh. Milioni 74.
Aliongeza kuwa watuhumiwa mbalimbali walikamatwa kwa kujihusisha na makosa ya kuhujumu miundo mbinu ya Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) na hatua za kisheria zitachukuliwa endapo watakutwa na hatia  na kufikishwa mahakamani

Kamishina Athumani amewaomba wananchi   kushirikiana na Jeshi la polisi  kwa kutoa taarifa pale wanapoona tukio la uhalifu kutoka kwa  mtu au kundi la watu likiingia nchini kinyume na sheria na pia kuwa makini wakati wanapoagiza magari  kutoka nje kwa kuwasiliana na ofisi za Interpol za ndani na nchi husika ili kuepuka usumbufu wa kukamatwa na gari za wizi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...