Moja ya eneo lililoaribika kutokana na hali ya mabadiliko ya tabianchi (Climate Change) katika fukwe ya Kilindoni, katika Kisiwa cha Mafia, Mkoani Pwani, nchini Tanzania. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).
Afisa Mazingira wa Wilaya ya Mafia, Bw. Gideon Zakayo.
Na Andrew Chale, Modewjiblog
[MAFIA-ISLAND] Kisiwa cha Mafia kijografia kipo karibu na mlango wa Mto Rufiji kusini mwa Tanzania.
Hata hivyo, Kisiwa hichi ambacho ni Wilaya moja wapo ya Mkoa wa Pwani inakabiriwa kwa kiwango kikubwa na changamoto za Mabadiliko ya tabianchi hasa baada ya wananchi wake wengi kutopata elimu hiyo sahihi.
Imeelezwa kuwa, elimu juu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi katika Kisiwa cha Mafia ambacho pia kinaunda visiwa vidogovidogo zaidi ya vitano, wananchi walio wengi katika kisiwa hicho bado hawajapata elimu sahihi ya kukabiliana na mabadiliko ya kimazingira (Climate Change).
Mtandao huu ambao ulipiga hodi katika kisiwa hicho cha Mafia ili kupata habari za mabadiliko ya tabianchi na namna ya Mabadiliko ya tabianchi yanavyo athiri Kisiwa hicho (How Climate Change effects Mafia Island in Tanzania) ambapo iliweza kuzungumza na maafisa Ardhi, Mazingira na wananchi wa Wilaya hiyo, na kueleza haya:
Kwa upande wa Afisa Mazingira wa Wilaya hiyo, Gideon Zakayo (pichani juu) amebainisha kuwa, Kisiwa cha Mafia kinakabiliwa na changamoto mbalimbali za Kimazingira ikiwemo hali ya Mabadiliko ya tabianchi huku suala la elimu kwa wananchi likiwa dogo kutokana na kutokuwa na fungu la kutosha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...