Mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Sunrise ya mjini Mwanza Janeth Malima akionyesha kipaji cha kucheza kwenye tamasha la Coke Studio lililofanyika shuleni hapo.

Wanafunzi wa shule za sekondari za Bwiru na Sunrise wakionyesha vipaji vyao vya kucheza na kuimba wakati wa tamasha la Coke studio.
Wanafunzi wakifuatilia burudani za tamasha la Coke Studio wakiburudika na kinywaji cha Coca-Cola

Mwanza,Dar,Mbeya na Arusha waonyesha vipaji vyao  vya kuimba
Msimu wa Coke studio mwaka huu ambao unajumuisha kolabo ya wanamuziki wa Tanzania na  wanamuziki kutoka nje ambao umezinduliwa mapema wiki iiyopita unazidi kuleta burudani katika makundi mbalimbali ya jamii ambao wanafunzi wa sekondari wamepata fursa ya kushiriki na kuonyesha vipaji vyao vya kucheza na kuimba.

Katika matamasha yaliyofanyika mwishoni mwa wiki  katika mikoa  ya Arusha,Mbeya,Mwanza na  Dar es Salaam wanafunzi kutoka shule mbalimbali waliweza kushiriki burudani za matamasha ya Coke studio na kuonyesha vipaji vyao vya kuimba na kucheza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...