Ibrahim Hassan Seushi
16 December 1948 – 25 July 2015

Familia ya Ibrahim Hassan Seushi, kwa moyo mkunjufu, tunapenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru ndugu, jamaa, majirani na marafiki wote waliofanikisha shughuli zote za msiba wa Marehemu Ibrahim Hassan Seushi ambaye alifariki katika hospitali ya Apollo, Chennai India tarehe 25 July 2015 na hatimaye kuzikwa tarehe 29 July 2015 Kituri, Mwanga.

Shukrani za pekee tunaomba ziwafikie wauguzi wa hospitali ya Muhimbili na Apollo, Eliamani Seushi, ndugu, jamaa na marafiki kwa kumhudumia, kwa sala, maombi na kujitokeza kwenu katika kutufariji na kututia nguvu.

Kwa kuwa ni vigumu kumshukuru kila mtu kipekee, tunaomba shukrani ziwafikie wote mliohusika kwa njia moja ama nyingine. Hatuna cha kuwalipa bali tunamwomba Mwenyezi MUNGU awajalie na kuwazidishia katika shughuli zenu za kila siku.

Pumzika kwa Amani, Mpendwa wetu, Baba yetu, Nguzo yetu.

Inna Lillahi wa inna ilayhi Raji un – Hakika, sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na hakika kwake tutarejea - Quran 2:156





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...