Baada ya mafanikio makubwa 2014, tamasha kubwa la muziki Karibu Music Festival lifanyikalo kila mwaka limerudi tena mwaka huu kwa kishindo kikubwa Novemba hii tarehe 6, 7 na 8.
Tamasha la Karibu Music Festival hufanyika kwa mfululizo wa siku 3 na litafanyika kwenye viwanja vya Mwakalinga Bagamoyo karibu kabisa na ufukwe wa bahari ya Hindi.
Mambo mazuri kwenye tamasha hili ni mchanganyiko wa mziki, utamaduni , michezo mbali mbali kutoka kwa wasanii mbali mbali watokao barani Asia, Ulaya , America na Afrika.Moja ya sababu ya kuanzishwa kwa tamasha hili ni kukuza na kutangaza mziki na utamaduni wa Afrika kwa nchi zingine. Miziki yenye asili ya pop, rock, Reggae, Hip Hop Jazz, country hupata umaarufu miongoni mwa wahudhuriaji.
 Mwaka huu watunzi na waimbaji watapata nafasi ya kuuza na kuoromote albam zao, pia wachonga vinyago na wasanii wengine watapata fursa ya kuonyesha kazi zao nzuri kwenye tamasha hili.
Kaymu Tanzania inakupa nafasi nzuri ya kuhudhuria tamasha hili la kipekee kwani tiketi zitauzwa kwa bei nafuu sana haijawai kutokea.

Kwa watu 50 wa kwanza watajipatia tiketi kwa Tsh 2,500 badala ya Tsh 5,000

Nunua tiketi yako kwa kubofya Kaymu.
Usisahau kumtaarifu na umpendae juu ya jambo hili jema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...