Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Mkuu wa MONUSCO, Bw. Martin Kobler akisisitiza jambo wakati wa mazugumzo yake na  Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania,  Balozi Tuvako Manongi. Bw. Kobler alifika katika Ofisi za Uwakilishi wa Kudumu, kuishukuru Tanzania kwa mchango wake wa ulinzi wa amani katika Mashariki ya DRC. Mchango ambao amesema umeleta tofauti kubwa.
"Tafadhali nifikishie salamu  na shukrani zangu  kwa Mhe. Rais, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Waziri wa Ulinzi" maneno ya  Bw. Martin Kobler kwa Balozi Manongi walipokuwa wakiagana  baada ya mazungumzo yao mwishoni mwa wiki. 

Na Mwandishi Maalum, New   York 
USHIRIKI  wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika Misheni ya  kulinda Amani ya Umoja wa Mataifa  katika  Jamhuri ya Kidemokrasi  ya Kongo ( MONUSCO), kumeelezwa kutoa mchango mkubwa katika kurejesha hali ya Amani na utulivu katika baadhi ya maeneo ya   Mashariki ya nchi hiyo.

Hayo yameelezwa mwishoni mwa wiki,  na  Mwakilishi  Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  katika  DRC na Mkuu wa MONUSCO  Bw. Martin Kobler, wakati alipofanya  mazungumzo na Balozi Tuvako Manongi,  Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.

Bw. Kobler  na ambaye alitumia fursa hiyo kuaga na kuishukuru  Tanzania kwa  ushiriki  na  mchango wake,  amesema,  katika maeneo mengi  ambayo walinzi wa Amani  wa Tanzania  wanayalinda hali ya Amani imerejea kiasi  ambacho wananchi waliokimbia  vita wamerudi na kuendelea na shughuli zako za kila siku.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...