Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) akimkaribisha ofisini kwake Mkuu wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu Tanzania kutoka Umoja wa Afrika (AU), Rais wa Zamani wa Msumbiji, Mhe Armando Emilio Guebuza. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (Katikati kulia) akimfafanulia jambo Mkuu wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu Tanzania kutoka Umoja wa Afrika (AU), Rais wa Zamani wa Msumbiji, Mhe Armando Emilio Guebuza (wapili kushoto), pamoja na wajumbe wenzake, jinsi Tanzania ilivyojipanga kuhakikisha Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu utakavyokuwa wa amani. Wakwanza kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mkuu wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu Tanzania kutoka Umoja wa Afrika (AU), ambaye pia ni Rais wa Zamani wa Msumbiji, Armando Emilio Guebuza (kulia) akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) wakati Mkuu huyo pamoja na wajumbe wenzake walipomtembelea Waziri Chikawe ofisini kwake kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu, hata hivyo, Chikawe aliwahakikishia kuwa Uchaguzi huo utakuwa wa amani. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil. Picha zote  na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...