2015-09-28
Jumuiya ya Watanzania Sweden
Mahali: Näsby Alle´6
183 55 Näsby Park
Siku: Jumamosi
Tarehe: 31-10-2015
Saa: 9:00 jioni
Kwa watanzania tunatoa taarifa ya wito wa Mkutano Mkuu wa ziada kwa ajili ya kuchagua viongozi watakao chukua majukumu ya kuwaongoza watanzania waishio nchini Sweden, na kujenga uhusiano na taasisi mabali mbali na vyama vyengine viliopo nchi jirani.
Uongozi wa kamati ya maandalizi ya Jumuiya ya Watanzania inawataarifu kwamba nafasi za uongozi huo ni kama zifuatazo;
Uenyekiti
Unaibu
Ukatibu pamoja na bodi ya utawala wa chama.
Tunawaomba watanzania wajutokeze kwa wingi katika mkutano huo ili tuweze kuboresha umoja wetu na kujenga maadili bora kwa watanzania, kujitolea kwenu ndio mafanikio ya taifa letu.
Asanteni
Kamati ya matayarisho
Asante kwa ujumbe.. Ila Huu umoja Uwe unafanya kazi kwa utaratibu mzuri.. AKIJA RAIS NA VIONGOZI WA SERIKALI YA TANZANIA MNAITA WATU WACAHACHE MKIDAI KUWA NI WAWAKILISHI WA VIONGOZI WA TANZANIA NA WAKATI SI KWELI KUNA WATU WALIALIKWA KWA KUJUANA. MJIREKEBISHE KATIKA HILI. MIMI NASEMA KAMA MTANZANIA NINAYEISHI SWEDEN NA HILI SIKULIPENDA. SALAMU ZIWAFIKE WANAOHUSIKA PAMOJA AN BALOZI.KAMA KWELI MANATAKA KUJENGA UMOJA WA KWELI WA WATANZANIA NCHINI SWEDEN NA NCHI ZA JIRANI MUWE MNAFANYA VITU KWA HAKI.MDAU- STOCKHOLM
ReplyDelete