Miss Tanzania 2013/2014 ,Happiness Watimanywa ambaye ni Balozi wa Saratani ya mlango wa kizazi kupia hospitali ya Marie Stopes( kushoto) na  Meneja wa Masoko wa hospitali hiyo Lilian Charles wakiingia kwenye uwanja wa taifa kutoa elimu kuhusiana na ugonjwa wa kansa ya kizazi wakati wa mchezo wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara kati ya Yanga na Azam, ikiwa nisehemu ya kampeni ya kuhamasisha akinamama kwenda kufanya uchunguzi wa saratani ya Kizazi kwanye vituo mbalimbali vya afya ikiwemo Marie Stopes.Ambapo timu hizo zilitoka sare ya 1-1.
 Balozi wa Saratani ya mlango wa kizazi kupitia hospitali ya Marie Stopes,Miss Tanzania 2013 /2014,Happiness Watimanywa(kushoto)akifafanua jambo kwa  Ofisa wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude(katikati) na Menaja masoko wa hospitali hiyo Lilian Charles(kulia)Kuhusiana na kampeni ya kuwahamasisha wakina mama kufanya uchunguzi wa saratani ya shingo na kizazi katika vituo mbalimbali vya afya. Uhamasishaji huo ulifanyika kwenye uwanja wa Taifa  jijini Dar es Salaa wakati wa mechi ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara kati ya Yanga na Azam ambapo timu hizo zilitoka sare ya 1-1.
 Miss Tanzania 2013/2014 ,Happiness Watimanywa,Ambaye ni Balozi wa Saratani ya kizazi kupitia hospitali ya Marie Stopes(watano toka kushoto)akiwa na maofisa wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF pamoja na Ofisa Udhamini na Matukio wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude(wa kwanza kulia) wakihamasisha kwa wakina mama kujitokeza kwenda kupima saratani ya kizazi katika vituo mbalimbali vya afya wakati wa mechi kati ya Azam FC na Yanga iliyochezwa mwishoni mwa wiki kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambapo timu hizo zilitoka sare ya 1-1.
Wachezaji wa timu ya Azam FC na Yanga sports Club wakichuna vikali wakati wa mechi yao ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara iliyopigwa mwishoni mwa wiki ambapo timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1.Kabla ya kuanza kwa mchezo huo Balozi wa Saratani ya mlango wa kizazi kupitia hospitali ya Marie Stopes,Miss Tanzania 2013 /2014,Happiness Watimanywa(hayupo pichani)alitumia frusa hiyo ya kuwahamasisha wakina mama kufanya uchunguzi wa saratani ya shingo na kizazi katika vituo mbalimbali vya afya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Uhamasishaji wa uchunguzi wa saratani za aina zote ni vizuri ufanyike hasa kwa wale waliozidi miaka arobainiwanahitaji kuchunguzwa kila mwaka. Usichelewe unapoona uvimbe mahali popote kwenye mwili wako wahi ukachunguzwe kama una saratani, pata matibabu mapema kabla ugonjwa haujasambaa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...