
Mwenyekiti
wa Mfuko wa Doris Mollel Foundation, Bi. Doris Mollel akiwakaribisha
wageni mbalimbali na wanahabari wakati wa utambulisho maalum juu ya
tamasha linalotarajiwa kufanyika siku ya Jumapili Novemba 8, katika
viwanja vya Leaders Club, jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Kaimu
Mkurugenzi Mkuu Idara ya Afya, uzazi na watoto, Bi. Georgina Msemo na
kulia kwake ni Dk. Sonal Peter ambaye ni daktari wa watoto
(Pediatrician) kutoka Hospitali ya Agha Khan. (Picha zote na Andrew
Chale, Modewjiblog).
Na Andrew Chale, Modewjiblog
[DAR
ES SALAAM] Katika kuadhimisha siku ya watoto njiti duniani, Taasisi ya
Doris Mollel Foundation (DMF) imeandaa tamasha la kwanza na la aina
yake kufanyika nchini siku ya Jumapili Novemba 8. 2015 kwenye viwanja
vya Leaders Club, Kinondoni kuanzia majira ya asubuhi mpaka saa 12 jioni
huku wasanii mbalimbali wakitarajiwa kushiriki kwa ajili ya kuchangisha
fedha za kununulia vifaa vya kusaidia watoto wanaozaliwa na uzito
pungufu ama watoto njiti.
Akielezea
mbele ya wanahabari jijini Dar es Salaam mapema jana, dhumuni la
tamasha hilo ni kuwaleta watanzania pamoja kupata uelewa na mwamko
katika kuadhimisha siku hiyo muhimu kwa afya na ustakabali wa mtoto
njiti ambapo kulingana na takwimu za Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,
takribani watoto 88,128 walizaliwa njiti au wakiwa na uzito mdogo nchini
kwa kipindi cha mwaka 2014/2015 pekee.
“Lengo
ni kuhakikisha kupitia Mfuko huu unasaidia watoto njiti hasa kwa vifaa
vya kuwawezesha kusaidia maisha yao. Tunataka kufikisha vifaa 10 kwa
kila Kanda chache za awali. Karibuni sana watanzania kwa siku ya
Jumapili Novemba 8. Kwa kiingilio cha sh 2,000 pekee kama mchango
ambapo utapata burudani ya kipekee kutoka kwa wasanii mbalimbali
wakiwemo Barnaba Classic, Mwasiti, kundi la The Voice, Miriam, Baraka De
Prince, Ruby, Shilole na wengine wengi.” Amebainisha Doris Mollel.

Tukio hilo likiendelea.
Aidha,
Doris amebainisha kuwa, Watanzania watapata fursa maalum ya kuusikia
wimbo ulioimbwa na baadhi ya wasanii hao watakaoshiriki katika tamasha
hilo.
DMF
imeongeza kuwa, baada ya tamasha hilo, kwa kushirikiana na wadhamini
pia itatoa vifaa mbalimbali ikiwemo (Suction machines, Oxygen
Concentrators na Feeding tubes) hii ni kwa Hospitali za Mikoa nchini
ilikuweza kusaidia watoto hao na vifaa hivyo vinatarajiwa kutolewa
katika siku ya kilele cha maadhimisho ya mtoto njiti Duniani huku kwa
Tanzania ikitarajiwa kufanyika Mkoani Mbeya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...