NA  BASHIR   YAKUB.
NILIWAHI  kueleza  namna ya  kuanzisha  kampuni   pamoja  na  usajili  wa  jina  la  biashara. Katika  makala  hayo  pia  nilieleza  tofauti  kati  ya   kusajili  kampuni  na  kusajili  jina  la  biashara.

  Hii  ilikwenda  sambamba  na  maelezo  ya  tofauti  za  kiuchumi   ya  vyote  viwili.  Ifahamike  kuwa  hizi  zote  ni  njia  za  kisasa  za  kujitafutia  kipato.  Makala  ya  leo  yanaeleza  namna   ya  kisheria  ya  kuanzisha   SACCOS.  

Tutaona  utaratibu  mzima  ambao   unaweza  kupitia  katika  kulifanikisha  hili.  Muhimu  ni  kujua  kuwa  SACCOS  nayo  ni  njia  kati  ya  njia  za  kisasa  za  kujipatia  na  kujiongezea kipato.  Aidha utaratibu  mzima  wa kuanzisha  na  kuendesha  SACCOS   unaongozwa  na  Sheria  namba  6  ya  2013  ya  vyama  vya  ushirika  ambayo  ndiyo  msingi  wa  makala  haya.

1.SACCOS  NI  NINI ?                                                                                                      
SACCOS   ni  kifupi  cha  neno  la  kiingereza  lijukanalo  kama  Saving  And Credit  CO-operative  Society.  Kwa  Kiswahili  kizuri  ni  chama  cha  ushirika  cha  akiba  na  mikopo.

  Kwa  faida  tu  ni  kuwa,  kwa  mara  ya  kwanza SACCOS  zilianzishwa  Ujerumani   na  mtu  aitwaye  Fredrick  Taylor.  Sura  ya  SACCOS   aliyoanzisha  Taylor  imekuwa  ikibadilika   kadri  shughuli  za  kijamii  na  kiuchumi  zinavyokua  mpaka  kufikia  aina  ya  SACCOS  zilizopo  sasa.

2.  SACCOS   KIUCHUMI.
Saccos  ni  asasi  ya  kifedha. Ni  muungano  wa  watu  ambao  lengo  lao  ni  kukusanya  fedha  na  kukopeshana  au  kufanya  biashara  moja  kwa  moja  na  kugawana  faida. Taratibu  za  kukopeshana  na  kufanya  biashara  katika  Saccos  hufanywa  na  watu   wenye  msimamo  au  fungamano  linalofanana.
Kusoma zaidi bofya  HAPA  AU  HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...