NA BASHIR YAKUB.
NILIWAHI kueleza namna ya kuanzisha kampuni pamoja na usajili wa jina la biashara. Katika makala hayo pia nilieleza tofauti kati ya kusajili kampuni na kusajili jina la biashara.
Hii ilikwenda sambamba na maelezo ya tofauti za kiuchumi ya vyote viwili. Ifahamike kuwa hizi zote ni njia za kisasa za kujitafutia kipato. Makala ya leo yanaeleza namna ya kisheria ya kuanzisha SACCOS.
Tutaona utaratibu mzima ambao unaweza kupitia katika kulifanikisha hili. Muhimu ni kujua kuwa SACCOS nayo ni njia kati ya njia za kisasa za kujipatia na kujiongezea kipato. Aidha utaratibu mzima wa kuanzisha na kuendesha SACCOS unaongozwa na Sheria namba 6 ya 2013 ya vyama vya ushirika ambayo ndiyo msingi wa makala haya.
1.SACCOS NI NINI ?
SACCOS ni kifupi cha neno la kiingereza lijukanalo kama Saving And Credit CO-operative Society. Kwa Kiswahili kizuri ni chama cha ushirika cha akiba na mikopo.
Kwa faida tu ni kuwa, kwa mara ya kwanza SACCOS zilianzishwa Ujerumani na mtu aitwaye Fredrick Taylor. Sura ya SACCOS aliyoanzisha Taylor imekuwa ikibadilika kadri shughuli za kijamii na kiuchumi zinavyokua mpaka kufikia aina ya SACCOS zilizopo sasa.
2. SACCOS KIUCHUMI.
Saccos ni asasi ya kifedha. Ni muungano wa watu ambao lengo lao ni kukusanya fedha na kukopeshana au kufanya biashara moja kwa moja na kugawana faida. Taratibu za kukopeshana na kufanya biashara katika Saccos hufanywa na watu wenye msimamo au fungamano linalofanana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...