Mkutano wa kila mwaka wa Kuwezeka umeme Afrika: Kongamano la Uwekezaji la Tanzania litafanyika Hyatt Regency Dar es Saalam, Hoteli ya Kilimanjaro kuanzia 3-4 Desemba 2015 

Mkutano ule utalenga siku za usoni za sekta ya kawi ya Tanzania kufuatia uchaguzi wa hivi majuzi, kutambua nafasi za uwekezaji na kubuni maushurikiano  muhimu kati ya wahusika kutoka sekta ya kibinafsi na ya umma. 
Dhibitisho za hivi karibuni za January Makamba, Mbunge wa Bumbuli, Tanzania, waakilishi kutoka Kitengo cha Rais cha Utekelezaji (PDB), Wizara ya Kawi, Madini na Kampuni ya Usambazaji wa Gesi (GASCO) zinaashiria juhudi zinazoendelea katika sekta ya umma  kuharakisha ufikiaji wa kawi nchini Tanzania kama  hatua muhimu katika ukuzaji wa uchumi. 
Hadi sasa, kampuni 37 za kipekee kutoka sekta ya kibinafsi zimedhibitishwa kuhudhuria ikiwa ni pamoja na Benki ya Uwekezaji ya Tanzania, Standard Chartered Bank, Mitsubishi Corporation, CitiBank Tanzania, BVI Consulting, Liquefied NG Tanzania, Statoil na Sunfunder. 
Yale mazugumzo yatalenga mijadala kama vile kujitolea kwa Tanzania kwa mageuzi ya sekta ya kawi, ukuaji wa kitengo hicho pamoja na ukuzaji gesi, mbinu za Tanzania za ununuzi katika sekta za kampuni za umma na umuhimu wa umeme kwa kilimo katika viwanda husika vya kuzalisha kawi. 
Kufuata ufadhili wa hivi karibuni wa dola za Marekani milioni $5 kutoka IFC kuwezesha Tanzania kuchunguza uwezo wa mitambo ya kawi iliyo ya nguvu za chini, mpangilio ule utachunguza pia njia mbalimbali za kupeana kupasisha kawi hadi nchini Tanzania na nafasi za kawi ya zitokanazo na jua, upepo, joto na maji, kama maendeleo ya ukuzaji wa kawi.



                                 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...