Abiria waliokuwa wanasafiri na basi la Burudani lenye namba za usajili T 572 BXJ kutoka jijini Dar Es Salaam kwenda Mashewa wilayani Korogwe mkoani Tanga na abiria wa vyombo vingine vya usafiri jana walijikuta wakikwama kwa masaa mengi katika eneo la Magoma baada ya mvua zinaoendelea kunyesha kwenye maeneo mbalimbali ya mkoa wa Tanga kuharibu miundombinu ya barabara huku mazao mengi ikiwemo mpunga na mahindi yakisombwa na mafuriko Picha na Vedasto Msungu wa ITV

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...