Nalimi Mayunga , mshindi wa shindano la Airtel Trace Music Stars Afrika, ameondoka nchini Jana kuelekea nchini Marekani kwa lengo la kupata mafunzo na kurekodi nyimbo yake 
Nalimi ameondoka usiku usiku wa kuamkia leo  kwenda kufanya kazi na nguli wa mzuki wa R&B nchini Marekani Bwana Akon ambapo anatarajiwa kukaa muda wa wiki moja kisha kurejea nyumbani tarehe 24 Novemba. 
Akiongea wakati halfa ya kumuaga, Afisa habari mwandamizi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Aristide Kwizera alisema” Tunajisikia furaha kuona vijana wa kitanzania wakitangaza sanaa na nchi yetu duaniani kupitia muziki. Napenda kumpongeza sana mayunga kwa kupata ushindi ambao umempatia nafasi hii nono na kumwomba atumie vyema fursa hii. Sisi kama wadau wakuu wa sanaa nchini tunawapongeza sana Airtel kwa kuanzisha program zenye lengo la kukuza sanaa na muziki wa nchini kama hii ya Airtel Trace Music Stars na nyingine nyingi. 
Naye mshindi wa shindano la Airtel Trace Music Stars Afrika, Nalimi Mayunga alisema” ile siku niliyokuwa naisibiria kwa hama leo imefika na nimejipanga kuondoka kwenda kujifunza mengi na ya msingi katika maisha yangu ya muziki . Naamini safari hii itakuwa ni ya mafanikio makubwa na mwanzo wa hatua yangu ya mafanikia katika tasinia ya muziki Napenda kuwaambia watanzania wajiandae kusikia kibao na video kali ntakayoifanya na Akon kwani nimejiandaa vya kutosha kuhakikisha nashirikiana nae vyema ili tunatoa nyimbo kali itakayowapa burdani wapenzi wa muziki pande zote duniani", aliongeza Mayunga 
Kwa upande wake Aliyekuwa jaji katika shindano la Airtel Trace Music Stars Tanzania na Mwalimu wa Muziki Tony Joet alisema” Mayunga amekuwa akifanya mazoezi kujiandaa kwa deli hii toka alipotangazwa mshindi wa Airtel Trace Afrika. 
"Nina imani naye kwani ameonyesha uwezo mkubwa na nidhamu ya hali ya juu na naamini atafika mbali na namtakia kila laheri katika safari yake” 
Akiongea kwa niaba ya Airtel Afisa Uhusiano wa Airtel bi Jane Matinde alisema” mipango yote ya safari imekamilika na mayunga atakuwa marekani kwa muda wa wiki moja, tunaamini mayunga atakaporejea atakuwa tofauti kabisa na alivyokwenda na ndio hasa lengo letu sisi Airtel, kuwawezesha na kuwainua vijana kubadilisha maisha na kufikia malengo yao. Shindano la muzuki la Airtel Trace Music stars lilizinduliwa octoba 2014 na huu ndio msimu wa kwanza wa shindano hili ambalo limewapatia vijana watanzania na waafrika nafasi ya kuonyesha vipaji vyao na kupata fulsa mbalimbali za muziki.
 Mshindi wa Airtel Trace Music Stars, Mayunga Nalimi  akiongea na waandishi (hawapo pichani) wakati wa tukio la kumuaga kwa ajili ya kwenda kurekodi video ya mziki na kupata mafunzo toka kwa  mwanamuziki wa kimataifa Akon nchini Marekani. hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika katika makao makuu ya ofisi ya Airtel Morocco jijini Dar Es Salaam. Pichani katikati ni   Afisa uhusiano wa Airtel Tanzania, Jane Matinde, akifatiwa na Mwalimu wa sauti Tony Joet.
Afisa uhusiano  na mwandamizi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Aristed Kwizera (kushoto) akimuaga mshindi wa Airtel Trace Music Stars, Mayunga Nalimi kwa ajili ya kwenda kurekodi  mziki na kupata mafunzo toka kwa  mwanamuziki wa kimataifa Akon nchini Marekani katika hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika katika makao makuu ya ofisi ya Airtel Morocco jijini Dar Es Salaam. Anayeshuhudia (katikati),ni Afisa uhusiano wa Airtel Tanzania jane matinde .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...