Mwanajeshi feki wa jeshi la wananchi(JWTZ)amekamatwa leo Mkoani Kigoma akiwa amevaa sare za jeshi hilo.

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake juu ya tukio hilo kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kigoma Fednandi Mtui alisema kuwa mwanajeshi huyo feki alikamatwa jana eneo la kazuramimba katika Wilaya ya uvinza.

Mtui alisema kuwa mwanajeshi huyo alitambulika kwa jina la James Charles miaka 27 mkazi wa kijiji cha Nyamori alikamatwa baada ya kuwepo kwa taarifa kutoka kwa raia wema juu ya utapeli aliokuwa akiwafanyia na kuwekewa mtego na kukamatwa.

Kamanda alisema kuwa mtuhumiwa huyo baada ya kuhojiwa na kuulizwa alipozitoa sare hizo alisema kuwa yeye ni dobi wa kufua nguo,hivyo huvaa sare hizo pale anapoletewa na wateja kwaajili ya kuzifua.

Alisema mtuhumiwa atafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika,pia jeshi la polisi limetia wito kwa wananchi wote ambao wameshatapeliwa na mtuhumiwa huyo kutoa taarifa katika kituo chochote cha polisi kilichopo jirani yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...