Baadhi ya Wagonja walifikishwa Hospitali hapo kwa ajili ya kupatiwa matibabu baada ya kupata maradhi ya matumbo ya kuharisha (kipindupindu).
Mwandishi wa Habari Rahma Suleiman akichukua maelezo kwa Mgonjwa aliyefika katika kituo hicho mara baada ya kupata hujambo.
Naibu Waziri wa Afya Mahmoudu Thabiti Kombo akionyesha ramani ya maeneo yanayoathiriwa zaidi na ugonjwa wa maradhi ya matumbo.
Naibu Waziri wa Afya Mahmoudu Thabiti Kombo akipata maelezo kwa Dkt. Dhamana Fadhili Ramadhan wakati alipotembelea wagonjwa wa maradhi ya kuharisha (kipindupindu) katika kituo cha Afya kiliopo Sheha ya Karakana.
angalau na nyie sasa mnatembea kujionea hali halisi, mlizoea kuambiwa tu, tinga tinga linakuja, fanyeni kazi jamani acheni mazoea ya ubosi wa paper work tu
ReplyDeleteMagufuli embu pita na hapo.
ReplyDeletePoleni sana mlioathirika na maradhi haya, Mwenyeez Mungu atawaafu na kuwajaaliya shifaa. Lakini jamani hicho kitanda cha mayowe (cha kamba) hivi mtu katika hali yake ya uzima keshawahi kukilalia bila ya mkeka au godoro? Au kwa vile hao ni wagonjwa na kwa pengine ndio weshakatiwa tamaa, inatilisha imani kwa kweli, kheri ukagaragara sakafuni kuliko hizo kamba zinavyoumiza. Sina hakika kama wamefanyiwa hivyo kwa maana maalumu, nisijekuwa nalaumu nikakosea. Poleni sana maradhi kuingia rakhisi lakini kutoka yataka stahamala. Uguweni pole jamani.
ReplyDeleteMahamoudu thabit kombo nI naibu waziri wa afya serikali ipi??
ReplyDeleteNadhani tuwe makini Mh Rais Magufuli hajatangaza hata Waziri Mkuu na Baraza lake.
Na kama ni wa zanzibar basi tufahamu serikali ya zanzibar haina mawaziri kwa sasa.
Kama ndugu kombo kashinda uwakilishi basi apewe heshima ya uwakilishi na sio u naibu waziri.
WAKUU WOTE Waende site sio kukaa ofisini. Rais hawezi tembelea maeneo yote na kwa kuwa watendaji wapo wafanye hiyo kazi vinginevyo mtamchosha rais wetu.ila pia Rais ashtukize Amana na Mwananyamala hospitsls
ReplyDelete