Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Dkt. James Mataragio akuzungumza mbele ya waandishi wa habari kuhusu ujio wa ndege ya pili ya utafiti wa awali wa mafuta na gesi asilia katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) mwishoni mwa wiki, ndege hiyo inatarajia kuanza utafiti wiki hii katika kitalu cha Eyasi Wembere na Mandawa.
Mkurugenzi Mtendaji TPDC Dkt. James Mataragio akipatiwa maelekezo ya jinsi ndege hiyo inavyofanya kazi (ndani ya ndege) kutoka kwa Meneja wa Mradi Brett Robinson wa kampuni inayoendesha utafiti huo ya “CGG AVITION LTD” katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), utafiti huo unagharamiwa na TPDC kutoka katika mfuko wa fedha za maendeleo.
Ndege ya utafiti wa awali wa mafuta na gesi asilia inayotarajia kuanza utafiti katika kitalu cha Eyasi Wembere na Mandawa ikiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) Mkoani Kilimanjaro mwishoni mwa wiki.
Meneja wa Mradi Brett Robinson wa kampuni inayoendesha utafiti huo ya “CGG AVITION LTD” (kushoto) akitoa ufafanuzi mbele ya waandishi wa habari jinsi ndege hiyo itakavyofanya utafiti, Mkurugenzi Mtendaji TPDC Dkt. James Mataragio (kulia).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...