Jengo la ujenzi wa kituo cha kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma.
  Sehemu ya jengo la ujenzi wa kituo cha kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma
  Sehemu ya jengo la ujenzi wa kituo cha kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mfuko wa NHIF, Michael Mhando akizungumza wakati wa makabidhiano ya  kituo cha kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma.
 Mkurugenzi mtendaji kampuni ya ujenzi Tanzania Building Works Ltd, Mohamed Iqbal Moray(kushoto), akimkabidhi funguo za  kituo cha kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa NHIF Michael Mhando.
 Mkurugenzi wa Fedha, Mipango na uwezeshaji wa mfuko wa NHIF, Deusdedit Rutazaa akizungumza wakati wa makabidhiano ya kituo cha kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma
Wafanyakazi wa mfuko wa NHIF na wa Hospitali ya rufaa ya Dodoma wakishiriki makabidhiano ya kituo cha kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma.

MFUKO wa Taifa wa Bima ya afya(NHIF) umekamilisha ujenzi wa kituo cha kisasa cha uchunguzi na matibabu kilichojengwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma ambacho kitasaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali hiyo.

Akizungumza katika makabidhiano ya jengo hilo, Kaimu Mkurugenzi wa NHIF,  Michael Mhando, alisema kituo hicho kitakuwa cha kisasa na kitatoa huduma mbalimbali ikiwemo huduma za CT-Scan na kitafunguliwa kabla ya mwezi januari mwakani ili

“NHIF umelipatia ufumbuzi tatizo la msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma baada ya kukamilisha ujenzi wa jengo hili ambalo limegharimu kiasi cha sh. Bilioni sita ikiwa ni pamoja na vifaa vya matibabu na samani,”alisema Mkurugenzi huyo.

Alisema ujenzi wa huo umeanza tangu mwaka 2008 na litakuwa na uwezo wa kuchukua vitanda 34 vya
wagonjwa.

“Kituo hichi kitakuwa na vyumba vya madaktari, maabara,  upasuaji, chumba cha kutolea dawa, mapokezi,  chumba cha wagonjwa mahututi, chumba cha dharura, mfumo wa miito ya wauguzi, na vifaa tiba vya kisasa,”alisema Mhando


Alisema kitatoa huduma kwa wanachama wa mfuko huo, wananchi wa Mkoa wa Dodoma na mikoa jirani.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...