Rais Jakaya Kikwete ateta na makamu wa Kwanza  wa Rais  wa Zanzibar Maalim Shariff Seif Hamad kuhusu hali ya kisiasa Visiwani leo  asubuhi  Ikulu jijini dar es Salaam
Wakiwa katika picha ya pamoja.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo Jumatano, Novemba 4, 2015, amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Chama cha Civic United Front (CUF), Mheshimiwa Seif Shariff Hamad ambaye pia alikuwa Mgombea Urais wa Zanzibar wa chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu uliofanyika Oktoba 25.


     Viongozi hao wawili walikutana kwa kiasi cha saa moja Ikulu,  Dar es salaam, kuzungumzia hali ya kisiasa Zanzibar kufuatia ombi la Mheshimiwa Hamad kutaka kukutana na kuzungumza na Rais Kikwete.

     Viongozi hao wamekubaliana kuwa mashauriano yaendelee kufanyika baina ya pande zote zinazohusika na hali ya kisiasa Zanzibar.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

4 Novemba, 2015






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...