Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akizungumza na Makatibu Wakuu, Manaibu Katibu Wakuu, Watendaji Wakuu serikalini leo Ikulu jijini Dar es salaam kupanga mikakati ya kuendesha serikali kwa weledi, nidhamu na moyo wa kupenda kazi.
Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika picha ya pamoja Makatibu Wakuu, Manaibu Katibu Wakuu, Watendaji Wakuu serikalini leo Ikulu jijini Dar es salaam baada ya kukutana nao na kupanga mikakati ya kuendesha serikali kwa weledi, nidhamu na moyo wa kupenda kazi.
PICHA NA IKULU
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA


Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli leo asubuhi
katika Ikulu ya Dar es Salaam amefanya
kikao na Makatibu wakuu, Manaibu Makatibu wakuu, Gavana wa Benki Kuu Prof.
Benno Ndulu na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kutoa uelekeo wa Serikali anayoitaka mara baada ya
kuapishwa.
“Nataka Serikali iendelee kwa nguvu zote
na katika kutekeleza dhana ya ‘HAPA KAZI TU’ na viongozi kuzingatia na
kukumbuka ahadi nilizotoa ili zianze kuonekana na kufanyiwa kazi mara moja” Rais
Magufuli amesema.
Katika Kikao chake, Rais ametoa mwongozo
na kusisitizia kuwa ni lazima kila mtendaji Serikalini kuuzingatia, kufuata sheria
na taratibu ili taifa lisonge mbele kwa ufanisi zaidi.
Katika kikao hicho Rais ameelekeza mambo
kadhaa ambayo watendaji hao wanapaswa kuyasimamia, kuyawekea mikakati na kuyapanga
vizuri ili atakapo teua Baraza lake la Mawaziri mambo hayo yawe tayari ili
Mawaziri watakaoteuliwa waweze kuyasimamia bila kukosa.
Mambo hayo muhimu ni kama ifuatavyo:
1.
Kuanzia mwezi Januari mwaka 2016, wanafunzi wote wanaoanza
shule watasoma bure bila kulipa ada, Katika jambo hili, Rais amewataka
watendaji kuanza kuliwekea mikakati tayari kwa utekelezaji
2.
Suala la mikopo ya wanafunzi nalo
lifanyiwe kazi na mipango yake ikamilike kwa ajili ya utekelezaji mzuri zaidi
3.
Amefuta safari zote za nje ya nchi
kuanzia leo hadi hapo atakapolitolea suala hilo maamuzi mengine na kueleza kuwa
shughuli zote zinazotakiwa kufanywa nje ya nchi zifanywe na kusimamiwa na mabalozi wa Tanzania wanaowakilisha nchi huko nje.
Pengine
patokee jambo la dharura sana na hata hilo lazima kibali kitolewe na Rais au
Katibu Mkuu Kiongozi. Badala yake Rais amewataka watendaji hao kufanya zaidi
ziara za kwenda vijijini ili kuzijua na kutatua kero za wananchi wa Tanzania.
Katika Kikao hicho, Rais amemtaka Kamishna
wa TRA, Ndugu Rished Bade kusimamia kwa makini zoezi la ukusanyaji wa mapato
nchini na kuhakikisha kero ndogo ndogo kwa wananchi lianze kutekelezwa kama
alivyo ahidi kwa kufanyiwa kazi mapema
zaidi.
Rais ameitaka TRA kukusanya mapato hayo
kutoka kwa wafanya biashara wakubwa zaidi na wale wanaokwepa kodi bila kuogopa
mtu wala taasisi yoyote hapa Tanzania na kusisitiza kuwa katika Serikali hii wa
kutoa maamuzi vinginevyo zaidi ya haya ni yeye Rais ama Makamu wake.
Rais Magufuli pia ameagiza usimamizi
katika suala la manunuzi ambalo limekuwa likitumika vibaya na kuwa mwanya wa
kuibia Serikali kwa watu kuongeza bei ya
vitu hata kama ni vya bei ndogo kabisa katika jamii.
“Ikitokea suala hilo likagundulika kwa
watu kuongeza bei ya vitu, watendaji watawajibishwa mara moja”. Rais
amesema, na kuwataka watendaji hao kufanya kazi zao kwa kuzingatia Sheria na
taratibu zilizopo na kuzingatia maadili mema ya kazi.
Imetolewa
na Premi Kibanga,
Mwandishi
wa Habari wa Rais, Msaidizi
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
7 Novemba, 2015
.
Nimeipenda hii. Naona ufisadi unaanza kuyoyoma.
ReplyDeleteMdau ughaibuni.
Umuhimu wa thana ya "HAPA KAZI TU" nchini ni sawa na umuhimu wa moyo mwilini. Japo mapapa waliyozowea kutula sisi samaki wadogowadogo watakwazika na dhana hiyo, lakini mapapa hao hawana hati miliki ya kumiliki nchi yetu wala kibali cha kutukoseshea mapato yakutuhudumia katika uchumi, elimu, afya n.k. Hivyo utekelezwaji wa dhana hiyo unahitaji kufanyika kwa spidi 700 kama ile ya ndege ya kivita.
ReplyDeleteUmeanza vizuri ndugu rais. Ukiendelea na mwendo huu, watanzania wataanzania tutaanza kunufaika na nchi yetu
ReplyDeletemisamaha mingi ya kodi wanapewa watu wa mashirika NGO na watu wa mashirika ya kidini , hii ifutwe pia kama kukusanya kodi iwe kwa wote sio kuwanyonya wafanyabiashara tu. Muache kuwanyonya watu wa rangi fulani fulani kuwa ndio wakutoa kodi na wa rangi nyengine wasitoe , usawa kwa wote. Na kutoa ruzuku kwa mashirika ya kikiristo peke yake pia ifutwe , au mashirika ya dini zote wapewe mgawo sawa kama makundi ya waisilamu , kuna wahindu , mabohora , mashia , ma agakhan nk huo ndio utakuwa usawa , au wote wasipewe. Serikali iliyoingia madarakani iache upendeleo kwa dini ya kikiristo , wafanyakazi asilimia zaidi ya 90 serikalini ni wao , jee hii ni haki na usawa? naomba Dk Magufuli aliangalie vizuri ili arekebishe kwa maarifa na vitendo.
ReplyDeleteSafi Sana magufuli waliokuwa Na tenda Za kifisafi Za viongozi kwishaa Watu wasiwe comfortable mfano kiongozi ticket yake NI $2000 kwasababu serekali hailipii Hapo Kwa Hapo Basi wajanja wanalipia Alafu wanachaji serekali $8000 per ticket piga viongozi wote WA serekali wanaosafiri NI billion ngapi zinapitea Hapo viva pombe
ReplyDeletepamoja na hayo yote, hiyo baraua pepe ya kutumia googlemail.com sijui ikoje. Kwa nini isitumike: ?
ReplyDeleteManake hiyo ya googlemail.com huenda ni ya bure na huku, pengine, ikulucommpress waliomba pesa za kulipia na kuendelea kulipia gharam ayake. I may be wrong!
The mdudu, Asante sana rais wetu haya ndio mambo tuyatakayo sasa wafanyakazi wote ndani ya Tanzania mjenge utamaduni wa kufanya kazi kwa kujituma na kwa uzalendo wa hali ya juu kabisa na muondokane na mambo ya vishawishi na uzembe mtu yeyote akikushawishi mfanye jambo baya huku ukijua unaweza kujikuta kwenye janga la kujitakia mlipoti huyo mtu kwa bosi wako ili uwe salama kabisa ni hayo tu kwa wafanyakazi wote hapo Tanzania sisi wote tuko nyuma yenu so pigeni kazi kwa mwendo wa HAPA KAZI TU
ReplyDeleteNaamin sasa tutanufaika na raisi wetu atalifikisha taifa sehemu mzuri na kuendeleza alipoishia dk kikwete
ReplyDeleteTunaiman kubwa sana na raisi wetu Dk magufuli atalifikisha taifa hili mahala.pa zuri na kuendeleza mema aliyoyacha dk jakaya
ReplyDeleteWe anon wa hapo juu. Tuliza boli. Naamini Magufuli ndo mtu anayeweza kuleta usawa kwa kuondoa imbalance ya ajira iliyopo baina ya wakristo na waislamu. pia atatoza kodi kiadilifu si kuwaumiza wahindi wakati wengine laa. pia ruzuku za dini zitarejewa upya (MOU). Pia mikataba ya madini nk.
ReplyDelete