NA MWANDISHI WETU,TANGA.

MKUU WA Mkoa wa Tanga,Mwantumu Mahiza ameutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mkoani hapa kuendelea kutoa elimu juu ya umuhimu wa wananchi kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ili kuweza kuongeza wigo mpana wa wanachama ambao wataweza kunufaika na huduma zao.

Alitoa wito huo jana wakati akipokea mashuka 150 yaliyotolewa na mfuko huo vyenye thamani ya shilingi milioni tatu yaliyotolewa na Mfuko huo kwa ajili ya vituo vitatu vya afya vya Mkinga, Maramba na Lanzoni vilivyopo wilayani Mkinga ambavyo zilikuwa zikikabiliwa na changamoto ya uhaba wa mashuka.

Kwa upande wake, Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu alimueleza Mkuu huyo wa mkoa kuwa dhamira yao kubwa ni kuhakikisha wanasaidia huduma za afya kwenye maeneo yalikumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa mashuka.

Aliongeza kuwa mikakati yao ni kuongeza ufanisi mkubwa katika kuwahudumia wananchi waliojiunga na mfuko huo ili waweze kupata huduma za uhakika wakati wanapokuwa kwenye vituo vya afya ili kuepukana na usumbufu usiowa wa lazima
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mwantumu Mahiza akipokea mashuka 150 kutoka kwa Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoani Tanga,Ally Mwakababu kwa ajili ya vituo vitatu vya Afya,Maramba,Mkinga na Lanzoni vilivyopo wilayani Mkinga mkoani hapa,Picha na Oscar Assenga.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mwantumu Mahiza akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya (NHIF) mkoani Tanga ofisini kwake mara baada ya kupokea mashuka 150 kwa ajili ya vituo vitatu vya Afya,Maramba,Mkinga na Lanzoni vilivyopo wilayani Mkinga mkoani hapa kulia ni Meneja wa NHIF mkoa wa Tanga,Ally Mwakababu na kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Salum Chima na anayefuatia ni Afisa Matekelezo wa (NHIF) Miraji Msile.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...