index
MWIMBAJI mahiri wa muziki wa Injili Afrika Mashariki na Kati, Ephraim Sekeleti amethibitisha kuwa mmoja wa waimbaji watakaopanda jukwaa la Tamasha la Krismasi na kushukuru linalotarajia kufanyika Desemba 25 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama Sekeleti amekubali kuwa mmoja wa waimbaji wa Kimataifa watakaopanda jukwaa la Shukrani ambalo litakuwa katika Sikukuu ya kumbukumbu ya kuzaliwa Masia, Yesu Kristo.

Msama alisema tamasha hilo ni la Shukrani baada ya kuombea amani uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, Tamasha la Maombi lilifanyika Oktoba 4 kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

“Tunarudisha heshima na Shukrani kwa Mungu baada ya kuiepusha Tanzania na majaribu yaliyokuwa na mlengo wa kutaka kuvuruga amani ambayo iliasisiwa na baba wa Taifa Mwalim Julius Kambarage Nyerere,” alisema Msama.

Aidha Msama alisema kuandaa tamasha hilo inaonesha namna gani Watanzania tulivyo na shukrani ambako Watanzania tukumbuke kwamba Tukipewa, Tusisahau kushukuru.

Ujumbe mzito ambao ni kumbukizi kwa Wanadamu ni kwamba binaadam tunapobarikiwa na Mungu hatuna budi kushukuru, hivyo tamasha hilo ni shukrani baada ya Mungu kusikia vilio vya Watanzania baada ya kuisaidia Tanzania katika uchaguzi Mkuu.   

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...