Katika mkakati wake wa kukuza ujasiriamali na ubunifu wa miradi endelevu nchini,Benki ya Stanbic imedhamini shindano la  Seedstars World kwa ajili  ya wajasiriamali wenye mawazo ya miradi endelevu ambalo limefanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Kwenye shindano hilo kampuni ya Juabar imeibuka na ushindi wa kushiriki kwenye shindano la ngazi ya kimataifa litakalofanyika nchini Uswisi mwezi Februari mwakani ambapo itawania kitita cha Dola za Kimarekani 500,000 kwa ajili ya kufanikisha uwekezaji inaotarajia kuufanya. Na gharama za ushiriki zitagharamiwa na Benki ya Stanbic.
Wazo la mradi wa kampuni ya Juabar ni kuanzisha teknolojia ya kusambaza vifaa vya kuchaji simu za mkononi kwa kutumia umeme wa jua ambapo vifaa hivyo maalumu vitasambazwa kwa watumiaji wa simu kwa gharama nafuu na kuwapunguzia adha wanayoipata kupata huduma hiyo kutokana na matatizo ya nishati ya umeme yaliopo hapa nchini. 
Akiongea kuhusiana na shindano hili kwa wajasiriamali Mkuu wa Kitengo cha huduma za biashara wa Benki ya Stanbic Tanzania Bw.Christopher Mlay amesema kuwa upo umuhimu mkubwa wa kuendeleza wafanyabiashara hususani wajasiriamali kwa ajili ya kukuza uchumi na maendeleo ya nchi.
 Alisema Benki ya Stanbic imejipanga kuwaendeleza wafanyabiashara nchini ambapo  imebuni huduma mbambali za kuwaendeleza na inafurahi kushirikiana na wadau mbalmbali wenye dhamira ya kukuza ujasiriamali na ubunifu wa miradi yenye tija inayoweza kuleta mafanikio kwenye jamii kama lilivyo shindano hili la Seedstars World.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa kampuni ya Juabar,Olivia Nava amesema anajivunia ushindi huo kupitia wazo la mradi wa nishati ya umeme wa jua na ana Imani itafanya vizuri kwenye shindano la kimataifa.
 Shindano la Seedstars World linazidi kupata umaarufu mkubwa kwa kusaidia kuendeleza wajasiriamali kutoka nchi mbalimbali duniani.Mwaka jana lilishirikisha makampuni ya ujasiriamali 36 ambapo mwaka huu itakutanisha wajasiriamali 53  nchini Geneva,Uswisi pia shindano hili limekuwa likilenga kuendeleza ubunifu wa matumizi ya teknolojia kwa makampuni machanga.
Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wa Benki ya Stanbic Christopher Gilbert Mlay (kushoto)akikabidhi tiketi ya ndege kwa mshindi wa  shindano la ubunifu wa zao la biashara kutoka kampuni ya Juabar Olivia Nava ambaye ni Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo ambaye atashiriki katika shindano hilo ngazi ya kimataifa litakalofanyika nchini Uswisi mwakani . Mshindi atajinyakulia kitita cha Dola za Kimarekani 500,000 kwa ajili ya kufanIkisha wazo lake la biashara wengine pichani ni ofisa wa kampuni ya Juabar Geofrey Shayo na kulia ni Gregory Pepper  kutoka kampuni ya SeedStar kanda ya Afrika.
Kwa maelezo zaidi tembelea:

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...