Katika kufikia ahadi yetu iliyopo kwenye malengo na dira ya benki ya kuwa taasisi ya fedha inayopendelewa zaidi nchini kupitia mtandao mpana wa matawi unaotoa huduma kwa gharama nafuu zaidi zenye kumlenga mteja na jamii ya watanzania,
Tunapenda kuwataarifu wateja wetu na umma kwa ujumla kuwa matawi yetu yote yatafungwa siku ya Alhamisi Novemba 5, 2015 ili kupisha sherehe za kitaifa za kuapishwa kwa Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Raisi wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Huduma zitarejea tena katika matawi yetu yote siku ya Ijumaa Novemba 6, 2015 kuanzia saa 2:30 asubuhi.
Ili kuhakikisha kuwa tunaendelea kukupatia huduma bora siku hiyo, njia mbadala za kibenki kama ATM, NMB mobile, NMB Wakala na Internet Banking zitaendelea kufanya kazi kama kawaida kwa masaa 24.
Hata hivyo, kituo chetu cha huduma kwa wateja kitaendelea kuwa wazi mpaka saa 2:00 usiku. Hivyo unaweza kuwasiliana na kituo chetu cha huduma kwa wateja kwa kupiga simu ya bure 0800 11 22 33 kwa msaada zaidi.

Imetolewa na Menejimenti ya NMB

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...