Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

JESHI la Polisi limewataka wananchi kuendelea na utulivu kama walivyoonyesha wakati wa upigaji kura na hatimaye kupatikana katika siku ya uampishwaji wa Rais Mteule Dk. John Pombe Magufuli.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Kamishina wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi hilo, Paul Chagonja amesema kuwa jeshi la polisi limeridhishwa na utulivu uliokuwepo wakati wa upigaji kura, na utulivu huo umeweza kufanya uchaguzi kwenda salama na hatimaye kukaweza kupatikana mshindi.

Amesema katika suala la Zanzibar liko katika mazungumzo na viongozi wanafanya kazi yao hivyo maandamano hayana nafasi kutokana na taratibu wanazozitumia.

Chagonja amesema watu waliokamatwa katika vurugu za uchaguzi wamefikishwa mahakamani na huku wengine wakiendelea na uchunguzi.

Amesema hali ya amani ipo na wananchi wametakiwa kulinda hali hiyo na ikitokea mtu analeta uchochezi walipoti kwa vyombo vya usalama ili hatua zichukuliwe.
Chagonja ametaka baadhi ya taarifa katika mitandao ya jamii kuupuzwa ,kwani zinatoa taharuki kwa wananchi na zinapotosha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...