Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kinondoni imeanzisha utaratibu kwa wananchi kutoa malalamiko juu ya watoa huduma katika manispaa hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda amesema kuwa kuna watendaji wanashindwa kufanya kazi ambazo waliziomba na kuifanya serikali ionekane ni kikwazo kwa wananchi wake.

Amesema kuwa baadhi ya wafanyakazi wanachelewesha kutoa huduma ili kutengeneza mfumo wa kupata rushwa na kusababisha shughuli nyingi za manispaa kushindwa kusonga mbele kutokana na waomba rushwa kazini.

Makonda amesema wananchi wanataka  huduma kwa wakati, kukosekana kwake kunafanya kuwepo kwa manung'uniko juu ya utendaji wa waajiriwa kwa kuweka mazingira ya kufanya kazi kwa kutegemea rushwa .

“Hatuwezi kuwa na wafanyakazi ambao kufanya kazi kwao mpaka wapate rushwa, wakati huku wanapewa mshahara na mazingira mazuri kwa mujibu wa sheria ya wafanyakazi katika serikali” amesema Makonda.  
 
Aidha amesema kuwa baada ya kupata malalamiko mengi dhidi ya idara au mtendaji hatua za nidhamu zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria ikiwa ni kutaka watumishi wafanye kazi   bila kuweka mazingira yenye rushwa.

Makonda amesema kukiwa na malalamiko dhidi yake ya utendaji wake yatakweda kwa Mkuu wa Mkoa, hiyo yote ni kuonyesha kila mtu kuwajibika kutokana na wajibu na utaratibu uliowekwa na serikali kwa watumishi wote.

Amesema kuwa wananchi wanaweza kutuma katika hatua hizi Kinondoni ,Maelezo dhidi ya huduma tatanishi, kwenda katika namba 15404 ambapo malalamiko yatapitiwa kila wiki na kazi hiyo inafanywa na vijana watano wenye ujuzi na kutoa majibu bila ya kumuonea mtu yeyote.

Makonda amesema baada ya miezi mitatu mtumishi au mtendaji kwa kazi aliyofanya ikiwa ya ufanisi atapata tuzo ikiwa ni kuonyesha kazi za serikali zinafanywa kwa mujibu wa sharia na kufuata maadili yaliyowekwa kwa ajili ya utoaji wa huduma kwa wananchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...