Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel inayoongoza kwa kutoa huduma za kibunifu imetunikiwa tuzo mbili za ubora za Tanzania Leadership Awards 2015 katika halfa iliyofanyika katika hotel ya Hyatt jijini Dar es salaam.

Airtel imejishindia tuzo hizo katika kipengele cha matumizi bora ya huduma za kimtandao kufikia wateja wake (best use of social Media in marketing) pamoja na kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji ya wateja (brand excellence) katika sekta ya mawasiliano na kuwashinda makapuni mengine yaliyokuwa wakichauana nayo katika kinyanganyiro cha tuzo hizo Wakionge wakati wa kukabidhi tuzo hizo , waandaaji wa tuzo hizo za Tanzania Leadership Awards, Kishore Bollakpalli alisema " Airtel imepata tuzo hizi kutokana na kufanya vizuri zaidi katika kuwasiliana na wateja wake kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii na hivyo kuwafikia wateja wake nchini nzima kwa urahisi zaidi.

Lakini kwa upande wa tuzo ya Brand excellence, Airtel imeonyesha kwa vitendo dhamira yao ya kutoa huduma bora kwa wateja wake huku ikitoa bidhaa na huduma za kibunifu ili kukidhi mahitaji ya wateja wake na kuboresha maisha yao.

Akipokea tuzo hizo Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Sunil Colaso alisema" Tunayofuraha kupokea tuzo hizi za Tanzania Leadership award na tunaamini huu ni ushuhuda kamili unaoonyesha kwa vitendo dhamira yetu ya kutoa huduma zenye zinazokidhi mahitaji ya wateja wetu zikiwemo huduma za intaneti, huduma za kifedha kupitia simu za mkononi na kuchochea kukua na upatikanaji wa huduma za kifedha nchini".

Colaso aliongeza kwa kusema Airtel itaendelea na dhamira yake yakutoa huduma zinazogusa mahitaji ya wateja wake u na kuwaweka karibu ili kuendelea kutoa huduma bora zaidi katika miaka ijayo.

Tuzo za Tanzania Leadership Awards zinalenga kutambua na kupongeza jitihada zinazofanya na watu binafsi na makapuni katika kuboresha uchumi wa Tanzania na maendeleo ya nchi kwa ujumla.
Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Sunil Colaso akipokea tuzo ya ubora katika kipengele cha kutoa huduma za kimtandao kutoka kwa waandaaji wa tuzo za Tanzania Leadership Award, Kishore Bollakpalli (kushoto). Airtel Tanzania imejishindia tuzo mbili za ubora katika kipengele cha kutoa huuduma za kimtandao pamoja na huduma zinazokidhi mahitaji ya wateja.
Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Sunil Colaso akionyesha tuzo mbili za ubora mara baada ya kukabidhiwa na waandaji wa Tanzania Leadership Award 2015. Airtel ilijishindia tuzo hizo katika kipengele cha kutoa huuduma za kimtandao pamoja na huduma zinazokidhi mahitaji ya wateja katika sekta ya mawasiliano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...