Balozi Modest Jonathan Mero, Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataiafa na Mashirika mengine ya Kimataifa Geneva na Vienna akiwasilisha hotuba ya Tanazania katika mkutano mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Viwanda Duniani ambao unajadili maendeleo endelevu ya viwanda kama njia mbadala ya kuzikwamua nchi maskini. Mkutano huu unafanyika jijini Vienna, Austria kuanzia tarehe 30 Novemba hadi tarehe 4 Desemba 2015.

Katika hotuba yake, Mhe. Balozi Mero, pamoja na mambo mengine aliwaleza wajumbe wa mkutano huo hatua mbali mbali ambazo zimekuwa zikichukuliwa na Serikali ya Tanzania kwa lengo la kukuza viwanda nchini ikiwa ni pamoja na mafanikio ambayo yamefikiwa hadi sasa.

Mhe. Balozi Mero pia alizungumzia juu ya mapitio ya Mpango wa Kitaifa wa Maendeleo wa awamu ya pili (National Development Plan Phase Two) ambao utatekelezwa na Serikali kuanzia 2016/2017 hadi 2020/2021 ambao pamoja na mambo mengine umeweka msisitizo wa kukuza viwanda kwa lengo la kuongeza thamani ya rasimali zetu, kukuza mahitaji ya ndani ya bidhaa za viwandani na kuongeza ajira kupitia viwanda, Sekta nyingine za uzalishaji, huduma duniani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...