Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi(watatu toka kushoto) na mkewe Marystella Masilingi (wanne toka kushoto) wakiwakaribisha Waheshimiwa Mabalozi mbalimbali wanaowakilisha nchi zao nchini Marekani kwenye mchapalo ulioandaliwa na yeye mwenyewe kwa ajili ya kujitambulisha kwao wakiwemo viongozi mbalimbali wa Jumuiya za Watanzania nchini Marekani, viongozi wa Dini, DICOTA na vyama vya siasa siku ya Alhamisi Desemba 10, 2015 kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani uliopo mtaa wa 22 jijini Washington, DC. Kulia ni Afisa Ubalozi Bi. Swahiba Mdeme. Picha na Vijimambo Blog/Kwanza Production
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi akisalimiana na Ben Kazora mmoja ya viongozi wa Jumuiya ya Watanzania Dallas, Texas mara tu alipowasili kwenye jengo la Ubalozi kuhudhuria mchapalo wa kujitambulisha kwa Mhe. Balozi Wilson Masilingi, watatu toka kushoto ni mkewe Marystella Masilingi na kulia ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme.
Afisa Suleiman Saleh akiwa kama mshereheshaji wa mchapalo huo akiwawakaribisha wageni na baadae kumkaribisha Afisa Swahiba Mdeme kwa ajili ya kumkaribisha Balozi Wilson Masilingi.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi akijitambulisha kwa Waheshimiwa Mabalozi na viongozi wa Jumuiya za Watanzania nchini Marekani kwenye mchapalo ulioandaliwa na yeye mwenyewe kwa ajili ya kujitambulisha kwao uliofanyika siku ya Alhamisi Desemba 10, 2015 katika Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...