Benki ya Exim Tanzania imetangaza kufunga mauzo ya dhamana yake ya muda mrefu (hati fungani) huku ikibainisha kuwa kiasi kilichopatikana kutokana na mauzo ya hati hizo kimezidi mara dufu (asilimia 195) ya malengo ya awali.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na benki hiyo jijini Dar es Salaam jana, uuzwaji wa dhamana hizo ulifungwa rasmi Disemba 18 mwaka huu huku benki hiyo ikifanikiwa kukusanya kiasi cha sh bilioni 19.7 kutokana na mauzo ya dhamana hiyo tofauti na makadilio ya sh. bilioni 10 iliyokuwa imejipangia kukusanya hapo awali.
“Awali lengo letu lilikuwa ni kukusanya takribani kiasi cha bilioni 10 hadi bilioni 15. Tunashukuru kuona kwamba tulichokusanya ni karibu asilimia 200 ya malengo yetu ya awali na kiasi kilichopatakina kimetoka kwa wawekezaji mbalimbali kutoka kila kona ya nchi,’’ alibainisha, Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki hiyo, Bw. Selemani Ponda.
Kupitia dhamana hiyo wawekezaji wanapatiwa uhakika wa kupata riba ya 14% kwa mwaka isiyokuwa na makato ya kodi,itakayolipwa kila baada ya miezi 6 kwa kipindi cha miaka 6 huku  ikiruhusu wawekezaji wenye kiasi cha kuanzia shilingi milioni moja.
Akizungumzia zaidi mafanikio hayo Bw Ponda alisema yametoa fursa kwa watanzania kuwa sehemu ya ukuaji wa benki hiyo huku akiongeza;“Mafanikio haya yanaonyesha imani kubwa waliyonayo watanzania kwa benki ya Exim na zaidi wanavutiwa na ubunifu wa benki hii katika huduma za kifedha.,’’

Bw Ponda alitumia fursa hiyo kuwashukuru baadhi ya wadau ikiwemo Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana nchini (CMSA), Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Wakala wa mauzo ya dhamana hiyo, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) pamoja na wawekezaji wote kwa kufanikisha mchakato mzima wa mauzo ya dhamana hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...