Mwanakamati wa Jumuiya ya Makanisa ya Kipentekoste (Tanzania Fellowship of Churches) Mchungaji Mchungaji Olivia Mallonga (kulia) akichangia mada wakati wa mkutano na waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo 22 Desemba, katika Ukumbi wa Idara ya Habari jijini Dar es Salaam kuhusu maandalizi ya Mkesha Mkubwa wa Kitaifa wa kuliombea Taifa pamoja na dua maaum ya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli ambaye anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika dua hiyo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Makanisa hayo Askofu Godfrey Malassy.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Makanisa ya Kipentekoste (Tanzania Fellowship of Churches) Askofu Godfrey Malassy akionyesha kitabu mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kilichozinduliwa na Jumuiya ya Makanisa hayo kinachohusu siri ya amani kwa taifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...