Timu kabambe ya soka ya E-FM imeufunga mwaka kimichezo kwa kipute cha dakika 90 za mpira wa miguu dhidi ya maveterani wa Boko Beach katika uwanja wa Boko Beach jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. E-fm ilifanikiwa kutawala mchezo katika kipindi cha kwanza na kuweza kuzitandika nyavu za Boko Beach Veterani mara mbili. 
Kasi ya mchezo ilibadilika katika kipindi cha pili baada ya E-FM kuandika bao lake la tatu kupitia nyota wake John Makundi. Bao  hilo liliamsha kikosi cha Boko Beach Veterani kwa kuutumia vizuri mpira wa adhabu kwa E-FM  kujipatia bao la kufutia jasho lililofungwa na mchezaji wake Kudra Omar. Na hadi mwisho wa mchezo E-FM  waliibuka wababe kwa jumla ya magoli 3-1
Picha ya pamoja ya kikosi cha E-fm
Picha ya pamoja ya kikosi cha cha Boko Beach Veterani 
Ibrahim Masoud Maestro akiambaa na mpira

Mlinda mlango wa Boko Beach Veterani akijaribu kuwapanga walinzi wake
Nahodha wa Efm Ssebo akitoka nje ya uwanja baada ya kulimwa kadi nyekundu kwa rafu ya bahati mbaya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...